Shirika la reli Tanzania limeufahamisha umma wa Watanzania kuwa huduma za usafiri wa treni za SGR zimerejea na kuendelea kama kawaida, likiomba radhi kwa wateja wake kwa usumbufu uliojitokeza, shirika likiwashukuru pia Wananchi kwa uvumilivu wao katika kipindi ambacho huduma za usafiri huo zilipotatizika kutokana na hitilafu iliyotokea mapema leo Alhamisi Oktoba 23, 2025.
Mapema leo Shirika la Reli Tanzania lilitoa taarifa kwa Vyombo vya habari likieleza kuhusu ajali ya Treni ya EMU iliyokuwa ikisafiri kutoka Dar Es Salaam kwenda Dodoma majira ya saa mbili asubuhi kutokana na hitilafu za uendeshaji, tukio ambalo lilitokea Kituo cha Ruvu na kwa taarifa za shirika hilo hakukuwa na athari kubwa za ajali hiyo.
0 Comments