Header Ads Widget

WANANCHI WA NGARA WAKUMBUSHWA KUWA AMANI NDO MSINGI WA MAENDELEO

Na Mariam Kagenda ,Matukio Daima Media, Kagera 

‎‎Wananchi wa Jimbo la Ngara mkoani Kagera wamehimizwa kuendelea kulinda amani iliyopo kwani amani ndo msingi mkubwa wa maendeleo 

‎Mgombea Ubunge wa Jimbo la Ngara  kupitia Chama cha Mapinduzi  Bwana  Dotto Jasson Bahemu amewakumbusha wakazi wa Jimbo hilo kutambua kuwa Amani  ndio nguzo kubwa ya maendeleo ya taifa.

‎Bw Dotto Bahemu amesema hayo kwenye  mkutano wake wa  kampeni  ikiwa ni mwendelezo wa mikutano hiyo yenye lengo la kuomba Ridhaa ya kuwa  Mbunge wa Jimbo hilo 

‎Amesema utekelezaji wa miradi ya maendeleo iliyoahidiwa kwenye ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) unategemea amani na utulivu wa taifa wakati na baada ya uchaguzi.

‎Bw Dotto Bahemu amewasisitiza  wakazi wa Jimbo la Ngara kukumbuka athari za kuvurugika Kwa Amani na Usalama kwenye Mataifa jirani hivyo hawatakiwi kuvuruga amani iliyopo .

Mgombea ubunge huyo amesema kuvurugika Kwa Amani nchini ni kuwakosea waasisi wa taifa akiwemo Mwl Julius Kambarage Nyerere na Hayati Sheikh Abeid Amani Karume.

‎Ameongeza kwamba wakazi wa Ngara hawatakiwi kushiriki katika vitendo  vyovyote vya uvunjifu wa amani kwani hata baada ya Uchaguzi wanatakiwa kubaki salama .


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI