Header Ads Widget

USALAMA WA ISRAEL HAUTISHIWI TENA BAADA YA KUPOKONYWA SILAHA KWA HAMAS-TRUMP

 

Baada ya kutua Tel Aviv na kufika katika bunge la Israel Rais wa Marekani ameanza hotuba yake kwa kutoa shukrani zake kwa Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, ambaye anamwita "mtu mwenye ujasiri wa kipekee".

Akizungumza akiwa Knesset Trump ametaja kuwa vita vya Gaza vilikuwa vikubwa kuwahi kutokea duniani na hatimaye vimefikia mwisho wake.

Tumeipatia Israeli silaha "isiyo na kifani" ili kufikia usawa wa nguvu na amani.

Pia ameeleza mbinu iliyotumika kuafikia yaliyoshuhudiwa leo.

''Hatutapigana vita "kwa busara" na tutafikia amani kwa nguvu'' anasema Trump.

Kama ilivyozoeleka Trump amejipiga kifua kwa kuwa kiongozi ambaye amesuluhisha vita vingi ambavyo watangulizi wake walishindwa.

''Nilimaliza vita nane katika miezi minane, na nitaongeza vita hivi vya Israel na Hamas kwenye orodha nitakapotia saini rasmi mjini Misri'', Trump aliongezea.

Baadhi katika umati wamesikika wakisema "Bibi" - lakabu ya waziri mkuu wa Israel.

Trump pia anashukuru mataifa ya Kiarabu ambayo yalisaidia katika mazungumzo.

Ni "ushindi wa ajabu" walifanya kazi pamoja, anasema. Sasa "itakuwa enzi ya dhahabu ya Israeli", Trump anaongeza, pamoja na "zama za dhahabu" kwa eneo zima.

Hotuba ya Trump ilikatishwa tu wakati MK (mbunge wa bunge la Israel) aliinua karatasi iliyosema "Itambue Palestina kama taifa huru".

Spika Amir Ohana alipaza sauti ya kutaka utaratibu huku kukiwa na pingamizi kubwa dhidi ya MK aliyekuwa akiandamana ambaye alitolewa nje haraka.

Ohana alisikika akiita jina la Ofer Cassif, mwanasiasa wa mrengo wa kushoto, lakini haijatambuliwa ni nani aliyetolewa nje.

Trump alianza tena hotuba yake akisema hiyo "ilikuwa nzuri sana".

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI