Tukirejea katika bunge la Israel ambapo Rais wa Marekani anatarajiwa kuhutubia baada ya ubadilishanaji wa mateka waliohai wa Israel na Palestina kukamilika, Waziri mkuu Benjamin Netanyahu amemshukuru Trump.
"Tunatambua jukumu muhimu ambalo Rais Trump amefanya katika kuwarudisha waliotekwa nyara," Netanyahu aliwaambia wanachama wa Knesset, na kuongeza, "Tumewarudisha wote waliotekwa nyara walio hai, na pia tumejitolea kurudisha miili ya waliofariki."
Netanyahu alipongeza msimamo wa Trump wa kuunga mkono Israel akisema, "Tunamshukuru Rais Trump kwa kutambua haki zetu za kihistoria katika Ukingo wa Magharibi na kwa kusimama dhidi ya uongo dhidi ya Israel kwenye Umoja wa Mataifa."
Alisisitiza kuwa "hakuna Rais wa Marekani aliyeifanyia Israel mambo mengi kama Rais wa Marekani wa sasa Donald Trump."
Netanyahu alielezea pendekezo la amani la Trump kama hatua "muhimu" kuelekea amani, na kuongeza, "Nimejitolea kwa amani hii, mmejitolea kwa amani hii, na tutafikia amani hii pamoja."
0 Comments