Header Ads Widget

PUTIN AONYA MAREKANI DHIDI YA KUPELEKA MAKOMBORA UKRAINE

 

Rais wa Urusi Vladimir Putin Alhamisi ameonya kwamba kupeleka makombora ya Marekani ya Tomahawk nchini Ukraine kutasababisha "kiwango kipya cha mashambulizi", pamoja na kuharibu uhusiano kati ya Urusi na Marekani.

Akizungumza katika mkutano huko Sochi, Putin alisema hilo halibadilisha hali ilivyo katika mstari wa vita, ambako Urusi inafikia maendeleo yake ingawa kwa mwendo wa taratibu inasonga mbele.

"Utumiaji wa makombora ya Tomahawk bila uwepo wa jeshi la Marekani ni jambo lisilowezekana. Hii itasababisha kiwango kipya kabisa cha mashambulizi, pamoja na uhusiano wa Urusi na Marekani, Putin alisema.

Kiongozi huyo wa Urusi alisema kuwa hata kama makombora ya Tomahawk yatasababisha uharibifu kwa Urusi ikiwa yatapelekwa Ukraine, ulinzi wa anga wa Urusi utaitikia haraka tishio jipya.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI