Header Ads Widget

MBUNGE WA AFRIKA KUSINI JULIUS MALEMA APATIKANA NA HATIA YA KUFYATUA RISASI HADHARANI.

 

Kiongozi wa Economic Freedom Fighters (EFF) Julius Malema hivi majuzi alitiwa hatiani kwa matamshi ya chuki

Mwanasiasa wa upinzani nchini Afrika Kusini Julius Malema amepatikana na hatia ya kufyatua risasi hadharani miaka saba iliyopita - kosa ambalo adhabu yake ni kifungo cha miaka 15 gerezani.

Mnamo 2018, video iliibuka ikimuonyesha kiongozi huyo wa Economic Freedom Fighters (EFF) akifyatua risasi kadhaa hewani wakati wa sherehe za kuadhimisha miaka mitano ya chama chake zilizofanyika katika jimbo la Eastern Cape nchini humo.

Alishtakiwa pamoja na mlinzi wake wa zamani Adriaan Snyman, ambaye aliachiliwa huru.

Malema alipatikana na hatia ya kutoa matamshi ya chuki chini ya miezi miwili iliyopita na mara nyingi huwasuta wazungu wachache katika nchi ambayo, miaka 31 baada ya ubaguzi wa rangi kumalizika, mivutano juu ya suala hilo inaendelea kujitokeza.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI