Kylian Mbappe alifunga amefunga magoli matatu katika mechi moja na kufikisha mabao 60 kwenye Ligi ya Mabingwa wakati Real Madrid ilipoichabanga Kairat Almaty nchini Kazakhstan.
Nahodha huyo wa Ufaransa alipiga mkwaju wa penalti dakika ya 25 baada ya kipa Sherkhan Kalmurza kumchezea rafu Franco Mastantuono.
Aliongeza mabao bao la pili dakika ya 52 alipouunganisha mpira wa Thibaut Courtois na kuuzamisha nyafuni. Dakika ya 73 Mbape akaweka nyavuni goli la tatu.
Wachezaji wengine waliofunga ni E. Camavinga (83') katika Brahim DÃaz (90'+3)
Ulikuwa ushindi wa 5:0 ulikuwa muhimu sana kwa kikosi cha Xabi Alonso baada ya kufungwa 5-2 na wapinzani wao wa jiji la Atletico Madrid kwenye La Liga Jumamosi.
Mabao hayo ya Mbappe kwenye Ligi ya Mabingwa – yanamaanisha amempiku mshambuliaji wa zamani wa Bayern Munich Thomas Muller na kuwa mfungaji bora wa sita katika historia ya mashindano hayo.
0 Comments