Header Ads Widget

MAMA SALMA KIKWETE AFUNGA KAMPENI JIMBO LA MCHINGA

 

Na matukio daima media

Mgombea Ubunge kupitia chama cha mapinduzi CCM Jimbo la Mchinga Mkoani Lindi Leo amehitimisha kampeni zake Kwa kunadi Sera za Chama hicho huku akiwasihi wananchi wa Jimbo hilo kuchagua viongozi wanaotokana na CCM kwani kina Ilani inayotekelezeka 

Ni tamati ya kampeni za Rais wabunge na Madiwani zikihitimishwa hapa Katika Kata ya Nangaru Manispaa ya Lindi ambapo Mama Salma Kikwete anawaahidi wananchi hawa kushirikiana nao Katika shughuli mbalimbali za Maendeleo ikiwemo ujenzi wa Kituo cha Afya Katika Tarafa hiyo 

Amesema chama cha mapinduzi kupitia Ilani ya ya Uchaguzi 2025/2030  inatambua tatizo hilo na ni miongoni mwa mambo yatakayoenda kufanyiwa kazi 

Salum Ng'ondo Ni Mgombea udiwani wa Kata hiyo ya Nangaru  Akatumia fursa hiyo kuwahimiza wananchi wa Kata hiyo kujitokeza kwa wingi siku ya tarehe 29 oktoba kwenda kukipigia Kura chama cha mapinduzi 

Kampeni hizo zilizoanza takriban miezi mwili iliyopita zimekuwa zikipokelewa kwa hamasa Katika vijiji na Kata za Jimbo Hilo la Mchinga ambapo wananchi wameonesha matumaini kwa Mgombea huyo wa Ubunge



Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI