Morogoro
MWANAMKE mmoja mwenye umri wa miaka 72, Amina Agustino mkazi wa Mtaa wa Nguzo,kata ya Mazimbu manispaa ya Morogoro, amefunguka kwa majonzi baada ya nyumba anayoishi kutangazwa kuuzwa kwa mnada kufuatia maamuzi ya Mahakama yaliyompa ushindi mumewe wa zamani Juma Khalifani katika kesi ya talaka.
Amina, anayelea watoto wawili wenye ulemavu,mmoja ulemavu wa akili na mwingine wa viungo, amesema hana pa kwenda endapo mnada uliopangwa kufanyika Novemba 7, 2025 utafanyika kama ilivyotangazwa na kampuni ya udalali wa mahakama Shashinhale Auction Mart.
“Naomba Serikali inione tu kwa jicho la Kipekee, sina pa kwenda na hawa watoto wangu wenye ulemavu wananitegemea mimi kwa kila kitu, saa 24 zote, umri nao umeshanitupa mkopo” amesema kwa sauti ya huzuni.





0 Comments