Header Ads Widget

ENG JOHNSTON MTASINGWA AWAGARAGAZA 4 KURA ZA MAONI BUKOBA MJINI

Na Mariam Kaagenda_Kagera 

Mhandisi wa TANROAD, Johnston Mtasingwa ameibuka mshindi katika Uchaguzi wa  Kura za maoni Jimbo la Bukoba Mjini  kwa kupata kura 1,408 na kuwabwaga wenzake  wanne waliokuwa wakishiriki mchakato wa kumpata Mbunge kupitia  Chama Cha Mapinduzi (CCM) 

Katibu wa Chama Cha Mapinduzi Jimbo la Bukoba Mjini, Shabani Mdohe ametangaza  matokeo ya kura za maoni ambapo amewataja wengine waliogombea kuwa ni Alex Denis ambaye amepata Kura  804 , Almasoud Kalumuna kura 640 Jamila Hassan kura 66 na Koku Rutha kura 44
             Mshindi wa Kura za maoni Jimbo la Bukoba Mjini (CCM) Eng Johnston Mtasingwa

 Wapiga kura waliojiandikisha ni 3033 waliojitokeza kupiga kura ni 2978 ambapo Kura  zilizoharibika ni kura 20 na kura halali ni 2958. 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI