Na Hamida Ramadhan, Matukio Daima Media Dodoma
Nyemo Selemona, mmoja wa wakazi wa Mbabala, alisema kuwa wapo tayari kumpigia kura mtu mwingine yeyote badala ya Mayala, hata kama ni jiwe, kwa madai kuwa hawajafaidika chochote katika kipindi chote cha uongozi wake.
“Kiukweli sisi hatupo tayari kuongozwa na Mayala tena. Kwa miaka kumi alikuwa diwani lakini hakuna hata sekta moja aliyogusa kwa maendeleo. Tupo tayari kupigia kura jiwe kuliko kumchagua tena. Leo hatuondoki hapa ofisini mpaka kieleweke,” alisema Selemona kwa hasira.
Naye Juditha Mgaya, mkazi mwingine wa Mbabala, alisema kabla ya kufanyika kwa kura za maoni waliwasilisha malalamiko rasmi kwa chama kuhusu kutomtaka Mayala, lakini hawakusikilizwa, hali inayoonyesha wazi kupuuzwa kwa sauti ya wananchi.
“Tulipeleka malalamiko yetu kwa maandishi tukiomba Mayala asirudishwe kugombea, lakini chama hakuchukua hatua yoyote. Tunajiuliza kura zenyewe zilihesabiwa vipi hadi akapitishwa?” alisema Mgaya.
Wakazi hao walidai kuwa iwapo CCM haitazingatia maoni ya wanachama wake wa ngazi ya chini, ipo hatari ya chama kupoteza mvuto kwa wananchi, hususan katika kipindi hiki kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu ujao.
0 Comments