Header Ads Widget

WABUNGE ROSE TWEVE NA NANCY NYALUSI WASHINDA TENA KURA ZA MAONI UBUNGE VITI MAALUM MKOA WA IRINGA

NA MATUKIO DAIMA MEDIA, IRINGA 

WABUNGE wa viti maalum mkoa wa Iringa Rose Tweve na Nancy Nyalusi wamefanikiwa kutetea nafasi zao kwa kushinda kwa kishindo kura za maoni. 

Akitangaza matokeo hayo Jana msimamizi wa uchaguzi huo Kheri James alisema kuwa Rose Tweve ameongoza kwa kwa kupata kura  554 huku Nancy Nyalusi akifuatia kwa kura 507 na mhandisi Fatma Rembo akishika nafasi ya tatu kwa kupata kura
326 . 

Nafasi ya Nne ikishikwa na Seki Kasuga aliyepata kura 152 na mwahabari Tumain Msowoya akipata kura 31.

Huku  Maria Makombe akipata kura 59 Libya Nzema Kura 25 ,Scola Mbosa akipata kura 8.

Wakishukuru baada ya uchaguzi huo Rose Tweve alisema kuwa anapongeza wajumbe kwa kumwamini na kuwa haya ni matokeo ya wajumbe na anasubiri maamuzi ya vikao vya juu huku akiahidi kuendeleza ushirikiano na wajumbe .


huku Nancy Nyalusi mbali ya kuwashukuru wajumbe alisema uchaguzi huo umekuwa wa haki na huru .


Mhandisi Fatma Rembo aliwapongeza wajumbe hao kwa kumpatia kura zaidi ya 300 kuwa ni kura nyingi na kuwataka wajumbe kuendelea kuhamasisha wanawake kujitokeza kwa wingi kumpigia kura Raia Dkt Samia Suluhu Hassan ,wabunge na madiwani wa CCM oktoba .














Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI