Iran imezionya Marekani, Uingereza na Ufaransa kutoisaidia Israel kukomesha mashambulizi ya kulipiza kisasi ya Tehran, kulingana na shirika la habari la Reuters likinukuu vyombo vya habari vya serikali ya Iran.
Ripoti zinasema kuwa Tehran italenga vituo vya kijeshi na meli zilizoko katika eneo hilo ikiwa nchi hizo tatu zitaiunga mkono Israel.
Waziri wa ulinzi wa Israel, Israel Katz, amesema "Tehran itaungua" ikiwa Iran itaendelea kurusha makombora.
Katika maoni yaliyotolewa wakati wa tathmini na maafisa wa kijeshi, Katz anasema: "Dikteta wa Iran anawageuza raia wa Iran kuwa mateka na kuunda ukweli ambao wao, haswa wakazi wa Tehran, watalipa gharama kubwa kwa shambulio la jinai dhidi ya raia wa Israel."
0 Comments