Siku ya Ijumaa, Urusi inatazamiwa kusherehekea gwaride la kijeshi la Siku ya Ushindi la kila mwaka huko bustani ya Red Square.
Mwaka huu, ni sawa na usitishaji mapigano nchini Ukraine, uliotangazwa kwa upande mmoja na Urusi mwezi uliopita.
Sherehe hiyo inaashiria ushindi dhidi ya Ujerumani ya Nazi mwaka 1945, na kumalizika kwa vita vya dunia vya pili huko Ulaya.
Umoja wa Kisovieti ulipoteza takriban raia milioni 27 wakati wa vita - zaidi ya nchi nyingine yoyote katika vita.
Kutokana na hali hiyo, Rais Vladimir Putin ametumia umuhimu wa kitaifa wa siku hiyo kukuza wazo la ushindi wa kishujaa dhidi ya ufashisti - kwa kuonyesha nguvu za kijeshi na vifaa vya Urusi.
Mwaka jana, mhariri wetu wa Urusi Steve Rosenberg aliripoti kwamba gwaride la kijeshi la kila mwaka la Red Square lilihisi tofauti, wakati wa vita nchini Ukraine.
"Tunaadhimisha Siku ya Ushindi wakati ambapo tunatekeleza Operesheni Maalum ya Kijeshi," Rais Vladimir Putin alisema katika hotuba yake.
"Wale wanaoshiriki kwenye mstari wa mbele ni mashujaa wetu."
0 Comments