Header Ads Widget

NIPO TAYARI KUFANYA KAZI PAMOJA NANYI KUFIKIA MALENGO YA MHE. RAIS – PROF. TUMAINI NAGU


Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI anayeshughulikia masuala ya afya Prof. Tumaini Nagu amefanyiwa mapokezi makubwa na viongozi, menejimenti na watumishi wa ofisi hiyo ambapo ameahidi ushirikiano ili kufikia malengo ya Serikali.

Prof. Nagu ameyasema hayo wakati akiongea na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI Bw. Adolf Ndunguru, baadhi ya viongozi, menejimenti na watumishi wa Ofisi ya Rais TAMISEMI baada ya mapokezi yake katika ofisi za Wizara zilizopo katika Mji wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma na kuomba ushirikiano na kuahidi kufanya kazi kwa pamoja ili kufikia dhamira na maono ya Mheshimiwa  Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Aidha, amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kumwamini na kumteua ili aisimamie Sekta ya Afya hususani Afya ya msingi chini ya Ofisi ya Rais TAMISEMI na amepokea kwa unyenyekevu mkubwa uteuzi wake na kuahidi kushirikiana kwa vitendo lakini anaamini uzoefu huongezeka kila siku na yupo tayari kufanya kazi na viongozi na watumishi wa ofisi hiyo.

Prof. Nagu afafanua kuwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alitoa maelekezo yake kwa kusisitiza kuboresha huduma za afya ya msingi, huduma ambazo zinatakiwa kuwafikia wananchi kwa wakati na dhamira yake ni kuyafanya mazingira ya afya kuwa bora, hivyo kama sehemu ya ofisi ambayo anakutana na wazoefu watamsaidia na kushirikiana naye ili kuyafanya hayo kwa vitendokwani kidole kimoja hakivunji chawa.


“lakini naomba itoshe sana kusema nakushukuru Katibu Mkuu (Bw. Adolf Ndunguru) pamoja nanyi nyote ambao mmenipokea siku ya leo, na hii ni ‘surprise’ kubwa, ishara kubwa kwamba mpo tayari kushirikiana nami na hilo ndilo ninaloliomba, tushirikiane ili tuweze kuwatumikia watanzania na yale maono ya Mheshimiwa Rais, basi yakatekelezeke kwa kumuunga mkono Rais wetu” alilisisitiza Prof. Tumaini Nagu 

Katibu Mkuu Adolf Ndunguru Ofisi ya Rais TAMISEMI Bw. Adolf Ndunguru amemkabidhi Kiongozi huyo Mpango Mkakati wa Taasisi na Muundo wa Ofisi ya Rais TAMISEMI na kusesema kuwa anamjua Naibu Katibu Mkuu (AFYA) Prof. Tumaini Nagu kama mtu mzoefu katika Sekta ya Afya na anaamini kuwa atafanya kazi nzuri na kwamba Ofisi ya Rais TAMISEMI yenye Idara na Vitengo 17 imempokea na itakuwa tayari kupokea maagizo yake na kuyafanyia kazi ili kuweza kufikia malengo na maono ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.   

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu Ofisi ya Rais TAMISEMI Bi. Emma Lyimo akitoa neno kabla ya Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI Bw. Adolf Ndunguru katika kikao kifupi cha menejimenti kumkaribisha Prof. Tumaini Nagu, amesema anayo furaha kubwa ya Kiongozi huyo mahiri kujiunga na familia ya Ofisi ya Rais TAMISEMI lakini pia kupata wasaa wa kukutana na kufahamiana na Viongozi, menejimenti na watumishi Ofisi ya Rais TAMISEMI.


 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI