Winga wa Manchester United na Argentina Alejandro Garnacho, mwenye umri wa miaka 20, ameonyesha dalili za kuondoka katika majira ya joto kwa kuiuza nyumba yake yenye thamani ya pauni milioni 3.85 miezi 12 tu baada ya kuinunua. (Sun)
Wolves wameshangaza baada ya kuibuka kutaka kumsaini winga wa Manchester United na England Jadon Sancho mwenye umri wa miaka 25, ambaye kwa sasa yuko kwa mkopo Chelsea, majira ya joto. (Football Transfers)
Mshambuliaji wa Lyon na Ufaransa Rayan Cherki, 21, ana kipengele kwenye mkataba wake cha kuuzwa kwa pauni milioni 25, huku Manchester United na Tottenham Hotspur wakiwa miongoni mwa vilabu vinavyomnyatia. (GiveMeSport)
Manchester United pia wanamnyatia mshambuliaji wa kimataifa wa Nigeria kutoka Atalanta Ademola Lookman, mwenye umri wa miaka 27, ili kutatua tatizo lao la uhaba wa mabao. (Caught Offside)
0 Comments