Header Ads Widget

CCM RUJEWA WAFANYA USAFI KUADHIMISHA MIAKA 48.

 


Na Josea Sinkala, Mbarali Mbeya.


Katika kuelekea maadhimisho ya miaka 48 tangu kuzaliwa kwa  Chama Cha Mapinduzi (CCM), wanawake wa Chama wa Chama hicho (UWT), wamejitokeza kufanya  usafi katika kituo cha afya Rujewa wilayani Mbarali mkoani Mbeya ili kuweka mazingira safi ya kutolea huduma za afya kwa wagonjwa na wananchi kwa ujumla.


Akizungumza kwenye zoezi hilo la kufanya usafi mmoja wa wanachama wa CCM ambaye ni mkazi wa mtaa wa Mbuyuni kata ya Rujewa

Rose Kinyaga, amesema wanamuunga mkono Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kufanya usafi katika maeneo ya hospitali na vituo vya afya ikiwa ni sehemu ya kaudhimisha miaka 48 ya kuwepo kwa chama hicho na kwamba mambo mengi yamefanywa na Serikali ikiwemo kwenye sekta za afya, elimu, barabara na nishati ya umeme.


"Hii siku kwetu ni maalum kabisa, tumetoka wanawake kufanya usafi hapa kituo cha afya Rujewa kwa maana ametujengea hospitali nzuri (Rais Samia Suluhu Hassan) na watumishi bora hivyo lazima tumuunge mkono tunaposherekea miaka 48 ya Chama chetu (CCM)", amesema Kinyaga. 


Katibu wa jumuiya ya wanawake wa CCM kata ya Rujewa Anna Mgonzi, amesema katika kuadhimisha miaka 48, ya kuzaliwa kwa CCM wanakwenda na Rais Samia Suluhu Hassan kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 kutokana na kazi kubwa anazofanya ikiwemo kupunguza vifo vya mama na mtoto kwa wilaya hiyo.


"Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi kwa ujumla tumejitokeza kuja kufanya usafi katika kituo cha afya kata ya  Rujewa, tumeona tuje tufanye usafi hapa ili kuweka mazingira safi na usalama wa  kituo chetu cha afya ambacho kimekuwa msaada mkubwa kwa wananchi", amesema Anna.



Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi kata ya Rujewa 
Karume Mungulu, amewashukuru wanachama wa chama hicho kwa kujitokeza kufanya usafi katika kituo cha afya na kwamba CCM ndiyo chama chenye dhamana ya usimamizi wa Serikali na kuwa kwa wilaya ya Mbarali hakuna kura itakayopotea kwa Rais Samia.

Jeremiah Makao ndiye Mheshimiwa Diwani wa Kata ya Rujewa, amesema kwamba wamefika katika kituo cha afya Rujewa ili kumuenzi Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika suala la utunzaji mazingira pia wameanza rasmi shughuli za miaka 48 ya kuzaliwa kwa CCM ambapo kiwilaya wataazimisha Februari 5, 2025 wakiungana na uongozi wa Chama hicho Taifa kuadhimisha sherehe hizo.

Makao, amesema maadhimisho hayo walianza Januari 30, 2025 ambapo jumuiya ya wanawake walianza usafi, jumuiya ya wazazi na umoja wa vijana walizindua mashina  pamoja na kutembelea miradi ya maendeleo, lengo kubwa likiwa ni kusherekea miaka 48 ya kuzaliwa kwa chama hicho sambasamba na kumpongeza Rais Samia kwa kazi nzuri ya kuleta maendeleo katika Taifa.

Diwani Makao, amewataka wanachama wa chama hicho kuendelea kushikamana ili waendelee kushika dola pamoja na kukijenga chama hicho  na kuwa na mshikamano wa pamoja na hatimaye kufikia maendeleo endelevu katika Taifa.




Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI