Header Ads Widget

BUNGUA MWEUSI ;YALITAWALA ZAO LA KAHAWA KAGERA.

 


Na Shemsa Mussa -Matukio Daima

           Kagera.

Maambukizi ya Bungua mweusi  yaendelea kulishambulia zao la kahawa Mkoani Kagera huku wananchi wakihofia kulipoteza zao Hilo 



Afisa  kilimo kutoka Halmashauri ya Bukoba  Babylus Mashauri akiongea katika kikao cha baraza la madiwani  amesema  halimashauri hiyo imepata  changamoto ya kisumbufu  kinachoshambulia Zao la Kahawa kinaitwa Bungua mweusi  wa Kahawa.

Mashauri  amesema madhara yake  ni kwenye matawi  ya Kahawa  anatoboa  matundu madogo  na kuingia ndani anataga mayai  kwaajili ya kuzaa.

Amesema Bungua  wa kiume  anaweza kuishi  siju 6 na Bungua wa  kike  anaishi  siku 58  na ana uwezo wa kutaga  mayai kati ya ( 20- 50 ) kwa uzao mmoja  lakini baada ya kuanguliwa hao wadudu  Bungua wa kike anakaa siku ( 19 ) kisha anaondoka kwenda kutafuta makazi mengine.

Amesema Athari za Bungua huyu ni kukauka kwa Matawi yaliyoshambuliwa na kadri anavyoendelea kushambulia  athari inaweza kuwa kubwa kupelekea kupoteza uzalishaji  kwa kiwango kinachoanzia  asilimia ( 20- 50 ) ya uzalishaji wa Zao la Kahawa.


Anasema mikakati ya kukabiliana na  ugonjwa huo ni pamoja na kuwajengea uwezo wa taalam wa kilimo kwa maana ya kuwatambua wadudu pamoja na madhara yake.

Amesema hatua ya pili ni kampeni kwaajili ya kumtokomeza mdudu huyo mwenye madhara makubwa kwa jamii inayojishughulisha na zao hilo kujiongezea kipato.


Anasema Zao la kahawa ndiyo kipaumbele kwa mkoa wa Kagera na ni Zao la kiuchumi  na kudai kuwa wapo kwenye mapambano ambayo kimsingi ni ya kiuchumi  kwa sababu Kahawa ndiyo uchumi wao.


Nae Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Erasto Siima wakati akifanya mahojiano na vyombo mbalimbali  baada ya kikao na Madiwani

amesema Tegemeo kubwa la mkoa na Wilaya ya Bukoba katika kukuza uchumi ni zao la Kahawa ambalo sasa umeibuka  ugonjwa  unaoshambulia mmea huyo.

" Hili jambo  ikiendelea  litashusha uchumk wetu, wataalam wa kilimo wameshasambaa  maeneo yenye mashamba ya kahawa kuangalia namna ya kufanya utatuzi,Nimeagiza wataalam wa kilimo kuangalia hasa maeneo yaliyo na uhalibifu  ili kuweza kushughulikia "anasema Mkuu wa wilaya hiyo.

Naye mwenyekiti wa Halmashauri ya Bukoba Murshid Ngeze ,amemuomba mkuu wa Wilaya kuwasaidia katika kukabiliana na tatizo la ugonjwa huo unaotishia maisha ya wakulima wa Kahawa.

Ngeze ,amewataka wataalam wa kilimo kutafuta suluhisho la haraka ili kudhibiti kabla  ya tatizo kuwa kubw kwenye jamii.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI