Mkuu huyo wa Wilaya alisema hayo mjini Morogoro katika wakati akikabidhi msaada wa vitimwendo 30 vya thamani ya shilingi milioni 10.5 vilivyotolewa kupitia yeye na msamaria mwema mmoja kutoka jijini Dar es salaam.
Kilakala akasisitiza jamii kuacha kuwaona watoto wenye ulemavu kuwa ni laana badala yake wawatoe na kuwapa huduma zote za msingi kwani wakiwezeshwa wanaweza.
Kwa upande wake Katibu Tawala wa wilaya ya Morogoro Bi Ruth John aliwaasa wazazi nao na walezi kukubaliana na hali ya ulemavu wa watoto wao kwani ni mapenzi ya Mungu na wasiwafiche badala yake wawatoe wapate huduma.
Aidha baadhi ya watu wenye ulemavu waliofaidika na msaada huo Seleiman Habibu, Juliana Kimungu anayemlea mjukuu wake mwenye umri wa Miaka kumi na moja Careen George na Rehema Senga ambaye ni mama Lishe walishukuru kwa msaada huo ambao sasa utawawezesha kusogea kutoka eneo Moja kwenda jingine wakati wowote bila shida ikiwemo wakati wa mvua ambapo hali huwa ni ngumu zaidi.
Rehema akasema katika shughuli zake za biashara ya mama lishe alikuwa akisogea kwa kusota na makalio lakini kitu alichopata kitamrahisishia na kuondokana na utegemezi
Wakashauri Serikali kuwapatia mikopo ilj kujikwamua kiuchumi kupitia asilimia kumi za kwenye halmashauri ambapo manispaa ya Morogoro imetenga shilingi bilioni moja na milioni 300 kwa wanawake, vijana na wenye ulemavu.
0 Comments