Na,Jusline Marco;Arusha
Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro kupitia maafisa waandamizi wake imeshiriki Shughuli ya utunzaji mazingira kwa zoezi la upandaji miti katika eneo la uwanja wa Magereza Kisongo jijini Arusha.
Afisa Mhifadhi Mwandamizi Idara ya Uhusiano wa Umma kutoka katika hifadhi hiyo Kasimu Nyaki akizungumza katika hitimisho la Tamasha la Land Rover lililoratibiwa na mkuu wa Mkoa wa Arusha Paul Makonda yaliyofanyika kwa siku tatu yenye lengo la utangaza utalii.
Nyaki amesema ushiriki wa NCAA katika zoezi hilo ni sehemu ya kuendana na Mabadiliko ya Tabianchi pamoja na kuhifadhi mazingira kama sehemu ya uhifadhi na utunzaji wa mazingira katika mkoa wa Arusha.
Katika hatua nyingine Nyaki ameeleza kuwa Mamlaka ya hifadhi ya ngorongoro imeshiriki kwenye tamasha la Magari ya Land Rover yaliyoratibiwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Paul Makonda ikiwa ni uungaji mkono juhudi za Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan za kutangaza Sekta ya Utalii Duniani.
Aliongeza kuwa NCAA kama wadau wa utalii matumizi ya gari aina ya Land Rover ni moja ya magari yanayotumika katika eneo la hifadhi kwenye shughuli mbalimbali za kiutalii na utafiti ambapo kupitia wizara mama ya maliasili na utalii imetumia fursa ma tamasha hilo kukutana na wananchi mbalimbali kutoa elimu kuhusiana na masuala ya uhifadhi na shughuli zinazofanyika ndani ya hifadhi ya ngorongoro ikiwemo vivutio vya utalii vilivyopo.
"Sambamba na utoaji wa elimu hiyo pia tunaelezea shughuli za maendeleo ya jamii ambazo tunazifanya ndani ya hifadhi ya Ngorongoro na nje,lakini pia kuelezea fursa za uwekezaji katika maeneo mbalimbali ndani ya hifadhi ya Ngorongoro."Alisema Afisa huyo
"Kwa ujumla tamasha hili limetupa nafasi kubwa ya kuendelea kukutana na wadau wetu hususani watalii wa ndani na nje pamoja na wananchi wa mkoa wa Arusha ambao wamekuwa wakitembelea katika tamasha hilo kupata elimu mbalimbali kuhusiana na masuala ya Utalii na tamasha hili limekuwa na manufaa makubwa sana katika kuwafikia wananchi kupitia shughuli mbalimbali."Alisistiza Kasimu Nyaki Afisa Mhifadhi Mwandamizi Idara ya Uhusiano wa Umma NCAA.
Awali Mkuu huyo wa Wilaya ameeleza kuwa siku tatu za Tamasha hilo zimekuwa na matokeo chanya kwenye uchumi wa Mkoa wa Arusha kwa wajasiriamali wadogowadogo na wafanyabiashara mbalimbali kutokana na ugeni wa watu zaidi ya 3000 ambao wamekuwa wakitumia fedha zao kwenye manunuzi na matanuzi.
0 Comments