Na Fadhili Abdallah,Kigoma
Msimamizi wa Uchaguzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu, Dk. Semistatus Mashimba ametoa maelekezo kwa wadau wa uchaguzi katika halmashauri ya wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma kutumia taratibu zinazoakisi 4R za Rais Samia Suluhu Hassan ili kuwezesha uchaguzi wa serikali za mitaa katika halmashauri hiyo kuwa huru, wa haki na shirikishi.
Msimamizi huyo wa uchaguzi ametoa maelekezo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwenye halmashauri hiyo katika mkutano uliohusisha viongozi wa vyama vya siasa,viongozi wa dini,wazee maarufu,vyama vya wafugaji na wakulima,watendaji wa vijiji na kata pamoja na waandishi wa habari.
Dk. Mashimba ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya Kasulu alisema kuwa ni takwa la kisheria lililomtaka kufanya hivyo ili wananchi wapate maelezo siku 62 kabla ya tarehe ya uchaguzi kwa lengo la kuhakikisha taratibu zote zinafuatwa kwa wapiga kura pamoja na wagombea kupata taarifa zote kwa wakati na kwamba 4R za Raisi Samia Suluhu Hassan ndiyo nafasi yake kufanyiwa kazi kikamilifu.
Msimamizi huyo wa uchaguzi alisema kuwa kampeni katika uchaguzi huo zitaanza tarehe 20 hadi 26 Novemba 2024 na uchaguzi utafanyika Novemba 27 mwaka huu ambapo amewaomba vyama vya siasa,viongozi wa dini na wadau wote mliopo kwenye halmashauri hiyo kudumisha amani na utulivu ili kuwezesha uchaguzi kufanyika bila changamoto yeyote.
Akizungumza katika mkutano huo Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kasulu, Abdallah Kazikwa ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika Daftari la Mkazi ambalo ni tofauti na zoezi lililopita la uandikishwaji katika Daftari la Kudumu la Mpiga Kura ili waweze kuitumia haki yao ya msingi ya kuchagua viongozi wanaowataka.
Kwa upande wake Katibu wa Baraza la Machifu Mkoa wa Kigoma,Abel Bussa ametoa rai kwa kila mwananchi mwenye sifa kujitokeza kugombea pamoja na kutoa ahadi ya kwenda kufundisha aliyojifunza kwa wengine juu ya umuhimu wa kupiga
Mwisho.
0 Comments