Header Ads Widget

MHANDISI MAHUNDI VIONGOZI UWT FA NYENI USAJILI WA WANACHAMA KWENYE WILAYA


Na Matukio Daima Media, Mbeya 


KATIKA kuelekea uchaguzi wa Serikali za mitaa viongozi wa umoja wa wanawake mkoa wa Mbeya(UWT)kufanya usajili wa wanachama katika wilaya zao ili kupata wawakilishi wengi katika uchaguzi mkuu 2025.


Kauli hiyo imetolewa Julai 11,2024 na Naibu Waziri wa Habari,Mawasiliano na Teknolojia ya Habari (Mb) Mhandisi,Maryprisca Mahundi wakati wa kukabidhi simu janja 15 kwa viongozi wa UWT mkoa wa Mbeya.


"Kila ofisi ya wilaya itapata simu mbili  pamoja na ofisi ya mkoa  kwa ajili ya kuhamasisha wanawake wapate usajili wa  kuwa wanachama wa UWT hii itasaidia kwenye uchaguzi mkuu  tuweze kupata uwakilishi mwingi"amesema Mhandisi Mahundi.


Hata hivyo Mhandisi Mahundi amewataka wanawake hao kuhamasisha wanawake wenzao  kujitokeza kwa wingi katika kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ikiwemo Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Vijiji ifikapo mwezi  Novemba  2024.


Pamoja na kukabidhi simu hizo pia Mhandisi Mahundi alichangia  Mil.10  kwa ajili ya Ujenzi wa ofisi ya Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Chunya ikiwa ni ahadi yake aliyokuwa ameitoa ya kuchangia  Mil.27  ,sambamba na hayo alitoa kanga doti 72 kwa Wajumbe walioshiriki Baraza la Umoja wa Wanawake (UWT) wilayani Chunya.


 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI