Na Matukio Daima Media, Mbeya
DIWANI wa kata ya Isyesye mkoani Mbeya,Ibra John amekabidhi sukari kilo 50 na majani ya chai kwa walimu wa shule tatu za msingi na Sekondari zilizopo katika kata hiyo zilizofaulisha kwa zaidi ya asilimia 90.
Diwani huyo ametaja shule zilizofanya vizuri kuwa ni Isyesye Sekondari,Ilomba shule ya msingi,Hayanga Shule ya msingi ikiwa ni sehemu ya motisha na kujali kazi kubwa iliyofanywa na walimu hao.
Motisha hiyo ya sukari kilo 50 na majani ya shillingi 10,000 kwa kila shule .
"Hii ni sehem ya mimi kama Diwani kutambua mchango wao katika kuelimisha wananchi wa Isyesye na Taifa kwa jumla
Shule zetu hizi kwa mwaka huu zilifaulisha wanafunzi kwa zaidi ya 90% hivyo tunawapa pongezi sana na waendelee na juhudi hizo ktk majukum yao"amesema Diwani John
Amesema kuwa kazi inayofanywa na walimu ni kubwa ni vema kutenga muda kuwashukuru hata kwa kidogo kinachopatikana ili kuwapa moyo wa ufanyaji kazi kwa bidii







0 Comments