Header Ads Widget

WEZI WA PIKIPIKI KATIKA SHEREHE ZA HARUSI, MISIBANI NA NYUMBA ZA IBADA MIKONONI MWA POLISI

 Jeshi la Polisi Mkoa wa Kusini Unguja linawashikilia watu wanne kwa tuhuma za wizi wa pikipiki katika maeneo ya mikusanyiko ya watu ikiwemo kwenye harusi, misiba na nyumba za ibada.

Akizungumza na waandishi wa habari  huko Tunguu Makao Makuu ya Polisi Mkoa wa Kusini Unguja Kamanda wa Polisi Mkoa huo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi SACP DANIEL SHILLAH amewataja watuhumiwa hao ni Iddi Abdalla Kisumba Miamkq 20 na Rashid Abdalla Sadala  Miaka  19 wakaazi wa Kidimni, Fakih Kassim Khamis  Miaka 19 mkaazi wa Amani na Ahmed Amour Abdalla Miaka 24 Mkaazi wa Makunduchi, ambao wamekamatwa katika maeneo tofauti wakiwa wameshaiba pikipiki tatu.

Aidha Kamanda shillah amesema wamefanikiwa kuwakamata watu wengine watatu ambao wanajihusisha na unyanganyi wa kutumia silaha kwa kuwavizia watembea kwa miguu huwatishia kwa mapanga na kuwapora kisha kukimbia kwa kutumia pikipiki, akiwemo Khalid Salum Said M. 20 Mkaazi wa Fuoni, Yassir Abdalla Shaaban M 30 Mkaazi wa Fuoni na Ali Mohamed Ali (Shetani Kiro)  M. 28 Mkaazi wa Kizimkazi Mkoa wa Kusini Unguja







Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI