WAKATI waumini wa dini ya kiislamu wakiwa katika mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan na wakristo wakiwa katika mfungo wa Kwaresma bei ya vyakula katika soko kuu la Manispaa ya Iringa imeendelea kuwa rafiki kwa wafungaji hao huku bei ya dagaa nyama nono ikipanda zaidi kwa kilo kuuzwa kwa Tsh 20,000 ukilinganisha na kilo ya nyama inayouzwa Tsh 8000.
Akizungumza na Matukio Daima Media Mariam Mahige ambae ni mfanyabiashara wa Dagaa katika soko kuu la mkoa wa Iringa soko la Manispaa ya Iringa alisema kuwa bei ya dagaa hizo maarufu kwa jina la Nyama Nono kutoka Mwanza imekuwa juu kutokana na upatikanaji wake kuwa mgumu na kuwa awali dagaa hizo zilikuwa zikiuzwa kati ya Tsh 14,000 hadi 17,000 ila kwa sasa zimekuwa adimu zaidi kutokana na walaji wengi kupenda kuzitumia .
Hata hivyo alisema dagaa nyingine kama aina ya Fulu na nyingine zinauzwa Tsh 16,000 pia dagaa hizo zinawawalaji wengi kwani wateja wa jumla wanakimbilia kununua dagaa hizo aina ya Fulu ambazo pia zinatoka Mwanza .
Ngowi Msungu ni mfanyabiashara wa Samaki katika soko hilo alisema bei ya Samaki wa kati ni Tsh 500 kwa mdogo kabisa na Samaki wa kati ni Tsh 5000 na kuwa Samaki wakubwa zaidi hawapatikani kirahisi na kuwa Samaki wa Tsh 5000 ni yule ambae wakati wa samaki wengi alikuwa akiuzwa kati ya shilingi 2500 hadi 3000 ila idadi kubwa ya walaji wa samaki wamekuwa wakilazimika kununua Samaki wachanga wanaopangwa kwenye mafungu kwa kuuzwa shilingi 1000 hadi 2000.
Wakati bei ya nyama katika maduka ya nyama (Bucha)mjini hapa kilo moja ikiuzwa Tsh 8000 na kilo moja ya utumbo ikiuzwa 6000 Maharage kwa kilo yamekuwa yakiuzwa kati ya shilingi 3000 hadi 2000 tofauti na miezi mitatu nyuma wakati bei ya maharage ilikuwa ikiuzwa hadi shilingi 2100 hadi 2200 alisema mfanyabiashara John Sanga kuwa bei ya maharage haijapanda kama wakati wa miezi ya Kilimo ambayo walaji walikuwa ni wengi kutokana na uhitaji wa mbegu na sasa sehemu kubwa maharage wakulima wameanza kuvuna .
Sanjari na bei ya mboga hizo ambazo hutumika katika mfungo wa kwaresma na mwezi mtukufu wa Ramadhani pia bei ya mchele kwa kilo katika soko hilo imekuwa ikiuzwa kati ya shilingi 2100 hadi 2800 tofauti na siku za nyuma ambapo mchele ulikuwa kati ya shilingi 1700 hadi 2000.
Wakati unga kwa kilo 25 ukiuzwa Tsh 30000 na kilo 5 ukiuzwa Tsh 7000 bei ambazo zilikuwa zikitumika wakati wote alisema Maria John mfanyabiashara wa mchele na unga sokoni hapo .
Mfanyabiashara wa ndizi na viazi mviringo katika soko hilo Hamida Kihongosi alisema bei ya ndizi mkungu ni kati ya shilingi 17000 na ndizi mzuzu zikiuzwa Tsh 30,000 bei ambayo wamekuwa wakiuza wakati wote wakati viazi kwa debe la lita 20 vikiuzwa tsh 15,000 na gunia wao wakinunua Tsh 60,000.
Wafanyabiashara wa Mihogo ,magimbi na viazi utamu sokoni hapo Isaya Mbalingwa na Obadia Isaya pamoja na Abnel Chuma walisema kuwa bei ya vyakula hivyo imekuwa ikiyumbishwa na hali ya upatikanaji wake kwa mfano mihogo ya Pawaga Iringa bei yake imekuwa kubwa ukilinganisha na mihogo ya Morogoro ambayo ina asili ya Kamba hivyo bei yake ni ndogo zaidi na kuwa bei ya mhogo mmoja ni kati ya shilingi 1500 na 2000 bei ambayo haina tofauti na kabla ya kuanza kwa mfungu wakati boga moja likiuzwa Tsh 2000 hadi 3000 .
Hata hivyo bei ya tambi kwa kilo moja katika soko hilo ikiwa juu zaidi kwa kuuzwa Tsh 30000 ukilinganisha na miezi miwili nyuma ambapo tambi ziliuzwa tsh 20,000 hadi 27,000 kwa kwa kilo .
Pamoja na wafanyabiashara wa vyakula hizo zinavyohusika na mfungo kudai kuwa bei ni kawaida baadhi ya wateja walisema bei hiyo ni kubwa ukilinganisha na hali halisi ya Maisha ya sasa kwani mhogo ambao umekuwa msaada mkubwa kwa wale waliopo kwenye mfungo bei yake si rafiki kwa mlaji tofauti na mwaka jana wakati kama huu wa mfungo mhogo ulikuwa kati ya shilingi 500 hadi 1500 bei ambayo haikuwa mbaya zaidi alisema Eliasa Juma .
Kuwa ni vema bidhaa hizo za mfungo kutazamwa kwa jicho la tatu ili zisimjuumize mlaji kwani hali ya upatikanaji pesa mfukoni si nzuri sana .
Monica Kalinga alisema bei ya vyakula si mbaya sana ila bei ya mboga mboga mfano dagaa ,Samaki ipo juu sana kwani kwa kawaida dagaa ni mboga ya hali ya chini ambayo awali ilikuwa kimbilio kwa wenye kipato cha nchini ila leo dagaa zimekuwa bei juu zaidi kuliko hata nyama jambo ambalo linashangaza zaidi kuona kilo moja ya dagaa ikiuzwa Tsh 20000 wakati nyama ikiuzwa Tsh 8000.
Akielezea hali halisi ya bei ya bidhaa sokoni hapo mwenyekiti wa Soko kuu la Iringa Raphael Ngulo alisema wanaishukuru serikali kwa kuthibiti upandaji holela wa bei katika masoko kwani bei ya vyakula vya mfungo ndani ya soko hilo haijapanda sana ukilinganisha na miaka mingine .
Alisema ukiona bidhaa imepanda bei zaidi ni kutokana na upatikanaji wake kuwa mgumu kwa baadhi ya maeneo miundo mbinu ya Barabara kuharibiwa na mvua hivyo kupelekea bidhaa kushindwa kutolewa mashambani na zile zinazofanikiwa kutolewa huuzwa kwa bei ya juu zaidi .
Hata hivyo alisema bei ya bidhaa za wafungaji wote zimekuwa rafiki zaidi mfano sukari ambayo ni hitaji kubwa kwa wafungaji hivi sasa inauzwa kati ya shilingi 3200 hadi 2800 tofauti na awali ilipokuwa ikiuzwa Tsh 6000 hadi 7000.
0 Comments