Header Ads Widget

BAADHI YA WAZAZI CHANZO CHA VIJANA KUWA NA MAISHA MAGUMU

 


IMEELEZWA  kuwa    ongezeko  la  vijana  wenye mazingira  magumu  katika  jamii  imesababishwa na  baadhi ya  wazazi na  walezi ambao kipato  chao  cha  chini  hivyo  kushindwa  kuwalea  vema  vijana  wao  kutokana na  fikra  mgando  waliziokuwa  nazo za kuishi  Maisha  ya kimasini wakati vijana  hao  wanao uwezo  mkubwa  wa kuzipambania  familia  zao  kuwa na Uchumi bora   kutokana na raslimali ardhi  walionayo vijijini .

Kuwa   ukifuatilia  chimbuko la  vijana   wenye mazingira  magumu unakuta linatoka  ndani ya  familia na  sababu  kubwa ni familia kukata tamaa na  kuona   kujimilikisha mzigo  wa  umasikini kama  ni  haki  ya familia   kuishi Maisha ya   kimasikini  pamoja na kuwa  na ardhi  nzuri  kwa  kilimo  jambo  ambalo  si  sawa .

Kwani   kwa  kawaida  ardhi ni mtaji  mkubwa  kuliko mali  nyingine   yoyote   na  ukiwa na ardhi unauwezo  wa  kufanya  maendeleo  makubwa nay a haraka  zaidi  kupitia  ardhi   tofauti na ukiwa na pesa pasipo  ardhi  .

“Tambua  pes ani  kila  kitu japo  ardhi  ni zaidi ya  pesa  maana  hata  mwenye  pesa ni lazima  kumtafuta  mwenye  ardhi  ili  afanya  shughuli za kilimo ama  uwekezaji hivyo  unaweza  kuwa na  pesa nyingi ila  ni lazima  ukatafuta mtu  mwenye  ardhi kama  ardhi  ni mtaji  hakuna  sababu ya  vijana  wanaotokana na familia  za  wazazi  wenye  ardhi  nao  kuishi  Maisha ya umasikini hasa  katika  nyakati  hizi  ambazo thamani ya  ardhi  ni  kubwa  zaidi “


Halfayo Mwalongo   mwanafunzi  wa  mchepuo  wa  ujasiriamali na  vitendo  na mkufunzi wa   mafunzo ya  ujasiriamali na vitendo  kutoka  chuo  kikuu  cha  Iringa  aliyasema  hayo leo   katika  ukumbi  wa  Yatima  wakati  wa  warsha   ya  kuwajengea  uwezo  wa  kiuchumi vijana  140  kutoka   vijiji vya  kata  tatu  za Mdabulo ,Ihanu na  Luhunga  katika  wilaya ya  Mufindi  mkoa  wa  Iringa  chini ya ufadhili  wa  mradi  wa  Youth Angecy Mufindi (  YAM).

Alisema   vijana  hao  wanatoka  ndani ya  vijiji  zaidi ya  15  vya  kata  hizo  tatu  hivyo  kupitia  mafunzo  hayo  watakwenda  kuwa  chachu  ya  vijana   na  familia  nyingine   kutokata  tamaa ya  Maisha  kutokana na  hali  duni ya kiuchumi   .

Mwalongo  alisema  wilaya  ya  Mufindi  ni wilaya  yenye  Uchumi  mzuri  ukilinganisha na baadhi ya  wilaya  hapa nchini  kwani  mazao ya  biashara  yanayostawi  katika  ardhi ya  wilaya ya  Mufindi ni fursa  pekee kwa  wananchi kuondokana na changamoto ya  kiuchumi iwapo  wataitumia  vizuri  fursa  hiyo.

Hata  hivyo  alisema   kwa  vijana  hao  wa mradi wa YAM ambao  wengi  wao  walionesha  kukata  tamaa ya Maisha  kutokana na hali  duni ya kimaisha katika familia  zao baada ya mafunzo hayo  watakwenda   kuwa  tofauti na  vijana   wenzao  ambao  hawajafikiwa na mradi   huo kwani mafunzo hayo  yatawafungua Kwenda  kuchangamkia  fursa  ardhi  inayowazunguka .

Alisema  kuwa  vijana  wengi  wamekuwa  wakikata  tamaa ya  kimaisha  kutokana na ugumu  wa Maisha kwa  kuhisi  kukosa mtaji  fedha  wa  kuendesha  Maisha  japo  wamesahau  kuwa  pesa  sio mtaji  pekee  bali ardhi  ni mtaji wa  uhakika katika  Maisha .

 

Hivyo  alisema  kutokana na mafunzo hayo wataweza  kutambua  fursa  zinazowazunguka  na  jinsi ya  kuzitumia   fursa  zinazopatikana katika  maeneo yao   kuelekea  katika  mafanikio  ya  kiuchumi pia  kuondokana na fikra  mgando  na  kuwa na  fikra  Chanya  za  kuwawezesha   Kwenda  kujitegemea   wenyewe .

  Mafunzo  haya  yamewapa uwezo  wa  kutambua   fursa  kubwa zinazowazunguka ambazo  mara ya  kwanza  hawakuweza  kuzitambua  kwani  wamepewa  uwezo  wa  kutambua  mitaji yao na  jinsi ya  kuipata  kutokana na mazingira  yanayowazunguka na  kupitia  mafunzo hayo  watakwenda  kuwa  chachu katika  familia zao”

Mwalongo  alisema kuwa  mradi  huo  wa YAM umekuwa  msaada  mkubwa kwa  vijana  hao  ambao  siku  zote walikuwa   wakilala  na kuamka  kwenye   fursa huku  Maisha  yao  yakiendelea  kuwa  duni pamoja na kuishi  familia  ya fursa .

Hivyo  alitaka  jamii kuepuka  kuwakatisha  tamaa ya  Maisha  vijana  kwa  kigezo  cha umasikini  wa  wazazi  wao kwani  umasikini  ni ugonjwa  unaoambukizwa ambao unaweza  kuikumba familia nzima  na  sio  lazima kuzaliwa  familia  masikini ni  sababu ya kila  mmoja  kuwa masikini  kwenye  familia kwa  kutumia fursa zilizopo  za  ardhi unaweza  kuzaliwa  kwenye  familia  masikini ila  wewe  ukawa tajiri  mkubwa .

Edina Mwagala  mkazi  wa  Kijiji  cha Ikanga  kata  ya Mdabulo ni  mmoja  wa  wanufaika  wa  mafunzo hayo alisema  wakati  anachaguliwa  kuingia katika  mafunzo  hayo ya  bure hakutambua  kama  atakuwa na upeo  mkubwa  wa kufikiri  kuwa na ndoto  ya  kuanza  safari ya  kujikwamua  kiuchumi  kupitia fursa  zinazomzunguka .

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI