Header Ads Widget

SONGAS YAKABIDHI VIFAA VYA MICHEZO NA FEDHA TASLIMU KWA AJILI YA UENDESHAJI WA LIGI VYENYE THAMANI YA MILIONI 34 KILWA

NA HADIJA OMARY, LINDI.

Kampuni ya kuchakata na kusafirisha Gesi asilia (Songas) imekabidhi vifaa vya michezo kwa kata ya Songosongo halmashauri ya Kilwa Mkoani Lindi vyenye thamani ya shilingi milioni 13 pamoja na fedha taslimu shilingi milioni 21 Kwa ajili ya uendeshaji wa ligi na tamasha la Michezo litalofanyika Desemba 1 siku ya UKIMWI duniani .


Akikabidhi vifaa hivyo  Meneja wa mradi ya kijamii wa kampuni hiyo  Nicodemus Chipakapaka amesema kampuni hiyo ya songas imekuwa ikijiwekea utaratibu wa kuchangia maswala mbali mbali kwa jamii  katika sekta ya michezo, afya na Elimu

Amesema wamekuwa wakifanya hivyo ikiwa ni sehemu ya kurejesha kwa jamii katika shughuli wanazozifanya pamoja na kutambua jitihada zinazofanywa na Serikali katika kuimarisha sekta hizo


Diwani kata ya Songosongo Hassan swalehe  Ameeleza kuwa vifaa hivyo vinakwenda kukuza na kuinua vipaji kwa vijana wa  kata hiyo ya Songo Songo

Kaimu Mkuu wa kitengo cha utamaduni sanaa na michezo Wilaya ya Kilwa Veneranda Kimaro amesema Katika kuendelea kukuza vipaji vya michezo kwa vijana tayari halmashauri imeshatenga bajeti ya ambayo inatekelezwa kupitia shughuli mbalimbali za kusimamia ligi kuanzia kwenye ngazi ya kata 


Baadhi ya Viongozi wa kata ya Songosongo  waliishukuru kampuni ya SONGAS kwa msaada huo walioutoa ambapo wamesema kuwa msaada huo  umeendelea kuimarisha ushirikiano baina ya wanajamii wanaozunguka eneo la mradi pamoja na kampuni hiyo ya Songas

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI