Header Ads Widget

HUKUMU YA MAJANE WA NYAMA YA SWALA ,USHAURI WATOLEWA


NA  FRANCIS   GODWIN , IRINGA

MAHAKAMA  zimeshauriwa  kabla ya  kutoa    maamuzi yake ya  mwisho  hasa  kwa  mwanamke  kukuangalia  sababu  juu ya  sababu ya  mwanamke  kufanya kosa  ndipo  itoe   hukumu  kwa  matakwa  na kwa  mujibu  wa  sheria  kuangalia  mahitaji ya  marekebisho  ya  yule  unayemtia hatiani .

Kuwa  hata  katika  misingi ya   viwango vya  kimataifa  vinasema  unapotaka  kumtia  hatiani  mtu aliyekosa  inataka  kuangalia  hitaji ya marekebisho  kwa  huyu  anayetakiwa  kupewa  adhabu kabla ya  kumpa  adha  ili  adhabu  iwe  kumrekebisha kuwa  mtu  mwema katika  jamii.

 

Akizungumza katika  mahojiano  maalumu  na Matukio Daima Media jana  ofisini  kwake   afisa  uangalizi   mfadhiwi  wa  mkoa  wa  Iringa  Hamis Jengela  alisema  kuwa  ofisi yake  inashughulika na utekelezaji  wa  adhabu  mbadala   wa  kifungo gerezani  alisema  kuwa   kuwa  pamoja na kuwa  uwezo  wa  ofisi yake  ni  mfungwa  aliyefungwa  kifungo  cha  miaka  isiyo  zidi  mitatu ndio  ambao  wanaweza  kumsaidia  kupata  adhabu mbadala  na  sio  aliyefungwa  zaidi ya  miaka  mitatu kama  ilivyo kwa  kesi ya Maria Ngoda  aliyefungwa  miaka 22 kwa  kosa la kukutwa nyara  za  serikali  ambayo ni  nyama  ya swala vipande 12.

Alisema  kuwa   hadi  sasa  ofisi yake  haijapata  kumsaidia  mfungwa  aliyefungwa  miaka  kama  hiyo ya Maria  Ngoda   japo  alisema  wamepata  kuwasaidia   wafungwa ambao  walifungwa kwa makosa ya  kuua bila  kukusudia na wengine  ambao  walihukumiwa kwa makosa ya  kuingia Hifadhini kinyume na  sheria .

Kuwa  ili  kupata  msaada  wa  huduma  za kijamii ni lazima  ombi  litoke  gerezani kwa  mkuu  wa  gereza na  ofisi yake  inakwenda  kufanya  uchunguzi  kwenye  jamii  ili kujua kama  kuna madhara  yoyote ya mhusika  iwapo  atapewa  adhabu  mbadala .

 

Jengela  alisema  kuwa mahakama  inapaswa  kuangalia  sana kabla ya  kumtia  hatiani  mtu  anayekosa   kuangalia  hitaji  la marekebisho  ila  wakati  mwingine mahakama  zetu  hazifikirii sana  katika  kutoa  adhabu kwa  wakosaji  .

“Ni  sahihi  sana  inapofika  hatua ya  kutoa  adhabu  kufikiri  sana  ili  kuangalia  adhabu  sahihi  ambayo itakuwa  hailengi  ukubwa wa  kosa  ila  inalenga  kumrekebisha mtu kuwa  raia  mwema  na  sio  kumkomesha “

Akijibu  swali la  mwandishi   juu ya  mtazamo  wa wengi  juu ya kesi  ya   malkia  ya pembe  za  Ndovu  aliyekutwa  na   vipande 511 vya meno ya Tembo  kupigwa   faini  alisema  kuwa  hapo  ndipo  anajikuta  akijiuliza  kwa  mahakama ya  Kisutu  iliyompiga  faini  malkia wa  vipande  511  vya meno ya  Tembo ilitazama  nini na  mahakama  ya  Iringa  iliyomfunga  Maria Ngoda  kwa kukutwa na  nyama ya  swala  vipande 12  iliangalia  nini .

Alisema kuwa wakati  mwingine mahakama  inapofika  hatua  ya  mwisho  kuangalia mahitaji  ya marekebischo ya  mtu unayemtia hatiani .

 

Hata   hivyo  alisema  kuwa  wakati mwingine  kwenye  utekelezaji  wa sheria  na maamuzi  huwa na mitazamo  tofauti kwa   watoa  haki  japo  asingependa  kushutumu mahakama  zote  kwani ni  vema  kuangalia kwa  kina  mahakama  ya  Kisuti  iliangalia  nini na mahakama ya  Iringa  ilitazama  nini kwani   sheria  inanalenga  kuadhibu  ,kumrekebisha ama  kumuonya mkosaji  hivyo vyete  vinawezekana .

Alisema  kuwa  kumekuwa na mitazamo  tofauti kati ya kesi ya  pembe za  Ndovu 511 na  adhabu  iliyotolewa na nyama ya Swala  vipande 12   kuwa na  adhabu  kubwa  zaidi .

Aidha  alisema  kuwa  toka  amekuwepo katika  ofisi  hiyo amejifunza  kuwa  kuwa  sehemu  sheria  imekaa vema  na  sehemu  sheria   hiyo hapo vizuri ila  kwa  upande wa  kulinda  raslimali za Taifa  anaona  sheria  imekaa  vizuri na  vema  jamii  kuepuka  kufanya makosa ya ujangili .

Pia  alisema  bunge  limetunga  sheria  nzuri  ya ujangili  na uhujumu  uchumi  ila  watendaji wa  mahakama  wanayo  nafasi ya  kuboresha   sheria  za bunge   Kwenda  vema  zaidi  na kuwa  watendaji  ni sehemu ya  sekretarieti ya   serilkali lazima kufanya kazi ya  kuisaidia  serikali na  kufanya kazi kwa  weledi  zaidi .

Alisema  kuwa  suala la kupewa  adhabu  mbadala  kwa mfungwa na  adhabu  kama  adhabu  nyingine kwani bado utakuwa mfungwa  isipo  kuwa utakuwa  mfugwa  huku  ukihudumia  familia  yako .

 

Sakata  la  Mjane Maria  Ngoda limeendelea  kuchukua  sura  mpya  kwa  jamii  kuonesha  nia ya  kumsaidia mjane  huyo   na tayari  umoja  wa wanawake Tanzania (UWT)  kupitia mwenyekiti  wake  Mary Chatanda  imejitokeza kutaka  kumsaidia  mjane  huyo  kumwekea  wanasheria  ili  kusaidia kumkatia  rufaa.

Katibu  Mwenezi wa  chama  cha mapinduzi (CCM)  mkoa wa Iringa Joseph Lyata  alisema  kuwa   CCM mkoa  wa  Iringa wamejinga  kufuatilia  familia yam jane  huyo  ili  kuona   namna ya kuisaidia na kama inazo  sifa  za  kuwepo kwenye  mpango wa kunusuru kaya masikini Tanzania (TASAF)  basi  kuingizwa katika mpango  huo na pia  kujua  sababu za mtoto wa mjane  huyo  kukatisha masomo ya  sekondari na ikiwezekana kumsaidia  kuendelea na masomo ya  sekondari.

Chama  cha mawakili Tanganyika  (TLS ) mkoa  wa Iringa  kimejitokeza  kumsaidia mjane   huyo pasipo gharama kwa  kupanga  jumla ya mawakili 10 ambao  watafanya kazi ya kumtetea mjane  huyo mahakamani .

 

Mwenyekiti wa  TLS mkoa wa Iringa Moses Ambindwile  alisema  idadi ya mawakili  imeendelea  kuongezaka na kuwa kuna  uwezekano wa mawakili  kuongezaka  zaidi na lengo la  TLS  kuona  mjane  huyo anasaidia  msaada wa  kisheria  na  kuwa  leo  Ijumaa watawasilisha mahakamani  ombi la kukata rufaa.

KU hiyo ilitolewa Novemba 3, mwaka huu na Hakimu Mkazi Mkuu Mkoa wa Iringa Said Mkasiwa baada ya kujiridhisha  kuwa ni kweli mjane huyo mwenye watoto wanne alikutwa na ndoo iliyokuwa na nyama hiyo yenye thamani ya Sh 900,000 kinyume na Sheria .

Akitoa hukumu hiyo kwa mjane huyo mkazi wa Zizi la Ng’ombe mjini Iringa, Hakimu Mkazi Mkoa wa Iringa, Mkasiwa alisema kosa hilo ni kinyume na kifungu cha 86 (1) (2) (c) cha sheria ya uhifadhi wa wanyamapori namba tano ya mwaka 2009 kama ilivyofanyiwa marekebisho na kifungu cha 59 (a) (b) cha mabadiliko ya sheria ya mwaka 2016.

Wakati akijitetea bila usaidizi wa wakili  mjane huyo alikiri ni kweli alikutwa na ndoo yenye nyama hiyo ambayo alidai alikabidhiwa na mtu aliyemtambua kwa jina moja la Fute bila kujua ina nyama ya nini .

Alisema alilazimishwa abebe ndoo hiyo na kufikishwa kituoni na kufunguliwa kesi ya kukutwa na nyara za serikali sambamba na kosa la uhujumu uchumi.

MWISHO 
  

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI