Header Ads Widget

UHABA WA MAFUTA WAKWAMISHA SHUGHULI ZA WANANCHI NJOMBE

 



Na Gabriel Kilamlya Matukio DaimaAPP NJOMBE


Serikali mkoani Njombe imeombwa kuingilia kati changamoto ya uhaba wa mafuta unaosababisha athari kubwa za kiuchumi na usafirishaji kwa wananchi.


Kutokana na kuadimika kwa Mafuta ya Petrol na Dizel Mkoani Njombe Watumiaji wa bidhaa Hiyo Wamesema kuwa Shughuli nyingi za Kiuchumi zimesimama na Hivyo kuathiri Vipato vyao vya Kila siku.



Mapema asubuhi Kituo hiki  kimeshuhudia Msongamano mkubwa wa watu katika Vituo mbalimbali vya Mafuta Mjini Njombe ambapo baadhi ya Watumiaji wa Bidhaa hiyo ambayo kwa sasa imekuwa adimu  akiwemo George Maltin  Wamesema kuwa Uhaba wa Mafuta umesababisha Shughuli nyingi za Kiuchumi kuyumba.


Kufuatia Uhaba Huo Wauzaji wa Mafuta Mkoani Njombe akiwemo Octavian Joseph Wamesema   Bidhaa Hiyo imekuwa adimu kwa sasa na Sio kwamba Wao Wamekuwa Wakificha Mafuta kama Baadhi ya Watu Wanavyosema.



Kwa upande wake Katibu Tawala Wilaya ya Njombe Agatha Mhaiki baada ya kufanya ukaguzi kwenye vituo mbalimbali vya mafuta wilayani hapa amekiri kuwepo kwa Uhaba wa Mafuta  na Kwamba tayari Wamesha ripoti Changamoto Hiyo katika mamlaka  husika.


Kila Jumatano ya mwanzo wa mwezi Mamlaka ya nishati na maji Nchini EWURA hutangaza bei mpya ya mafuta iwe kupanda ama kushuka jambo ambalo wengi wanaamini baada ya kutangazwa mafuta huenda yakaanza kupatikana.



Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI