Header Ads Widget

UANZISHWAJI WA MIRADI YA MBWAMWITU NA FARU WEUSI WAFANYA ONGEZEKO LA WATALII MKOMAZI


Na Pamela Mollel - Matukio Daima App, Mkomazi.


Kutokana na  kuanzishwa  kwa miradi ya wanyama adimu ya  Mbwamwitu na Faru weusi  katika hifadhi ya Taifa ya Mkomazi, wageni  wanaelezwa  kuongezeka  kwa asilimia 100 katika kipindi cha mwaka  2022/2023  katika hifadhi ya Mkomazi jambo ambalo limechangia ongezeko la  mapato


Hayo yamebainishwa na Mhifadhi Mkuu anaesimamia kitengo cha Utalii Happyness  Kiemi wakati akielezea mafanikio waliyoyapata kwa waandishi wa habari waliotembelea hifadhi hiyo hivi karibuni ambapo amesema hayo yametokana na uhamasishwaji uliyofanywa na hifadhi kutokana na kuwepo kwa vivutio hivyo adimu


Kiemi ameeleza kuwa bado wana matarajio ya kuongezeka kwa  wageni hususan wageni wa ndani na ongezeko hilo pia limetokana na uwepo wa  filamu ya Royal Tour iliyozinduliwa na Mh.Rais.


“Hifadhi yetu bado ina matarajio ya kuwa na ongezeko la wageni hususan wageni wa ndani ambao wanakuja kutazama Faru na Mbwamwitu na katika kipindi cha miaka miwili ijayo tunatarajia wageni kuongezeka zaidi”.Alifafanua Kiemi.


Kwa upande wake Mhifadhi mwandamizi  anaesimamia miradi hiyo ya wanyama adimu Emanueli Sisya ameeleza kuwa  hifadhi ya Mkomazi ilichanguliwa kama hifadhi ya uzalishaji Mbwa mwitu kutokana na eneo hilo kushabihiana na mazingira  wanayoishi mbwa hao


Sisya  amefafanua kuwa mradi huo ulianza ukiwa na mbwa mwitu 25 ila kwa sasa wameongezeka na kufikia zaidi ya 300 ambapo huwaachia mbwa hao katika mifumo ya kiiolojia na kwa sasa  lengo lao ni kuzalisha na kuwarudisha katika maeneo yao ya asili

“Mbwawitu ni wanyama wanaoishi kimakundi,”Yaani kifamilia hivyo tunawaachia katika makundi tukiangalia mbwamwitu wenye umri unaolingana”.Alifafanua Sisya


Aidha amezitaja faida zinazotokana na mbwamwitu kuwa  ni kivutio kikubwa cha utalii hususan kwa  wageni  ambao wengi wamekuwa wakitembelea hifadhi hiyo kutokana na  uwepo  wa kivutio hicho cha mbwa mwitu,na hivyo wana mpango wa kuendelea kutanua kwa kujenga boma lingine ili kuwezesha wageni kuendelea kuwaona na utalii kukua


Kwa upande wake Mratibu wa wanyama hao adimu  Jackson Lyimo akazitaja  Changamoto kubwa wanazokabiliana nazo mbwamwitu  kuwa  ni pamoja  na  migongano baina ya wafugaji  na  wanyama hao kwa kuwa wanawaona kama wanyama waharibifu


Lyimo amefafanua  kuwa  tangu  kuzalishwa kwa  mbwamwitu  katika hifadhi ya Mkomazi  tayari wameachia makundi 15 yenye mbwa zaidi 209 ikiwa ni kurudisha  ikolojia ya hifadhi ya  Mkomazi kwa kuwarudisha  katika hifadhi ambazo zilikuwa na mbwamwitu  ila wakatoweka kutokana na sababu mbalimbali


“Mbwa hawa pia wanakutana na changamoto za magonjwa pindi wanapokutana na wanyama wakufugwa lakini pia binadamu ni adui mkubwa wa wanyama hao kwa kuwa wanamuona kama mharibifu”.Alifafanua Lyimo.


Mradi wa mbwa mwitu katika hifadhi ya Mkomazi  ulianzishwa mwaka 1995 ukiwa na lengo la kuzalisha  mbwa mwitu na kuwarudisha katika maeneo yao ya awali kutokana na kuendelea kutoweka kutokana na sababu mbalimbali


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI