Header Ads Widget

JESHI LA POLISI LAKAMATA WATUHUMIWA 97 NA PIKIPIKI 111 PAMOJA NA WAHAMIAJI HARAMU

 



JUMLA ya watuhumiwa 97 wamekamatwa kwa tuhuma za wizi wa pikipiki 111 na mali mbalimbali. 


Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na jeshi hilo kwa vyombo vya habari na kamanda wa polisi mkoani Pwani ACP Pius Lutumo alisema hayo ni mafanikio kwa kipindi cha mwezi Agosti.


 Lutumo ametaja aina na idadi ya pikipiki hizo kuwa ni Haoujue 23, Boxer 30, Fekon 10, SanLg 16, Sinray 1, Kinglion, Senke 01, bajaji 4 na Tvs 23 mali zidhaniwazo kuwa za wizi.


Pia kwenye matukio mengine jeshi limefanikiwa kukamata Bhangi viroba 7, Puli 60, Kete 791 na Mbegu za Bangi kilogramu 5, Mirungi Kilogramu 5, Bunda 3 za mirungi ambapo umla ya watuhumiwa 114 wamekamatwa katika makosa hayo.


JESHI la Polisi Mkoa wa Pwani limewakamata wahamiaji haramu watatu toka nchi mbalimbali kwa kuingia nchini bila ya kibali.

 

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na kamanda wa polisi mkoani Pwani ACP Pius Lutumo imesema kuwa watuhumiwa hao wamekabidhiwa Uhamiaji kwa hatua za kisheria.


Lutumo alisema kuwa watuhumiwa hao ni kutoka nchi za Ethiopia mmoja, Kenya mmoja na Uganda .

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI