Header Ads Widget

HATUA KALI ZA KISHERIA KUCHUKULIWA KWA WANAOKAIDI KUFANYA USAFI NJOMBE

Saada Milanzi afisa afya mkoa wa Njombe
Mkurugenzi Halmashauri ya mji wa Njombe Kuruthum Sadick
Afisa mtendaji kata ya Njombe mjini Enosy Lupimo

Na Gabriel Kilamlya Matukio DaimaAPP NJOMBE

Ili kuepukana na magonjwa ya mlipuko kikiwemo kipindupindu na magonjwa ya kuhara wananchi mkoani Njombe wametakiwa kuacha tabia ya kutupa taka ngumu kwenye mabonde yanayotiririsha maji.


Agizo hilo limetolewa na Afisa Afya wa mkoa wa Njombe Saada Milanzi katika zoezi la ufanyaji usafi lililojumuisha mamia ya wakazi wa halmashauri ya mji Njombe katika mtaa wa National Housing.


Aidha Enosy Lupimo  Ofisa Mtendaji wa Kata ya Njombe Mjini ambaye anasema wameunda kikosi kazi cha watu watano kwenye kila ubalozi kwa ajili ya kufuatilia suala la usafi huku watakaokaidi kutekeleza agizo la usafi hatua kali za kisheria zitachukuliwa.


Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Njombe, Kuruthum Sadick ameonya tabia ya baadhi ya watu wanaotupa taka hovyo mitaani.


Kwa upande wao baadhi ya wananchi mkoani Njombe akiwemo Zuwena Msemwa wamelaani kitendo cha baadhi ya wanaokwenda kutupa taka  kwenye maeneo yasiyostahili.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI