Header Ads Widget

MWENYEKITI UVCCM MOSHI VIJIJINI RASMI AUAGA UKAPERA...

 Na Gift Mongi MATUKIODAIMA APP MOSHI

Sasa rasmi mwenyekiti wa umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi(UVCCM)wilaya ya Moshi Vijijini Yuvenail Shirima ameuaga ukapera.

Ilikuwa siku nzuri hapa maeneo ya Kilihome akisherehekea maamuzi haya yakubadilishwa jina na kuitwa mume bàdala ya yale majina 'baby,my,honey'

'Tumefurahi kumuoma kijana mwenzetu akisherehekea ndoa yake na Mungu amtangulie katika haya majukumu mazito'anasema Geofrey Munisi

Sherehe hii ya aina yake imefanikiwa kuwakutanisha watu wa kada tofauti tofauti ambapo pia ilifana mithili ya ujio wa Masiya ambapo ilikuwa pia ni gumzo.

'Ndio tumefurahi kumuona mwenyekiti wetu anauaga ukapera ni jambo zuri sana tumtakie kila la kheri katika maisha haya mapya anayoyaanzisha'anasema


Wakili Emanuel Mlaki anasema ndio ni jambo jema na hivyo mwenyekiti huyo ameonyeshwa njia kwa vijana wanaogopa ndio

Anasema kuwa ndoa ni heshima kwa jamii lakini pia ni Baraka kutoka kwa Mungu na kuwa lazima iheshimiwe.

'Vijana wengi wanaogopa ndoa na hili lazima tuweke sawa ni mpango wa Mungu na uzuri lipo katika maandiko lazima tuheshimu'anasema


Fatuma Mwende anaongeza mwenyekiti huyo kwa kufunga ndoa na kuwa hii inatoa taswira ni jinsi gani kijana anatakiwa kuwa picha ya anaowaongoza.

'Ukiona kijana anafikia hatua ya kuwa na mwenzi ndani yaani mke uje ameshakomaa kiakili tayari hivyo hata maamuzi yake yatakuwa na busara'anasema

Mwisho

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI