Header Ads Widget

MILLARD AYO NA HAMISA MOBETO WAMWAGA MAMILIONI KWA WASHINDI WA TIGO CHA WOTE

Ikiwa ni mwendelezo wa kampeni ya chawote ya Tigo  imekabidhi washindi sita hundi ya milioni moja moja  ofisini kwao Jijini Dar es salaam

" Leo tunayo furaha kubwa kuwa na baadhi ya washindi wa Wiki ya Nane wa Kampeni ya TIGO CHA WOTE ambao hawa ni washindi wa Milioni Moja Moja kila mmoja, Lakini niwakumbushe Watanzania kwamba kila siku CHA WOTE inatoa zawadi ikiwemo pesa taslimu hadi Milioni Moja kwa washindi 320 kila siku , kuibuka mshindi ni rahisi tu unachotakiwa ni kufanya miamala na Tigo Pesa kama Kutumia Lipa Kwa Simu , Kununua Vifurushi , Kulipia Bili kwa Tigo Pesa , n.k kwa kufanya ivyo nawewe siku si nyingi utakua miongoni mwa Washindi wa Kampeni hii ya CHA WOTE , Hadi sasa Tigo wameshatoa Zawadi ya Pesa kUANZIA Milioni Moja hadi Milioni Tano kwa Watanzania Takribani 21160 nafasi bado ipo ya kila mtu kuibuka mshindi " Walisema Mabalozi wa Kampeni iyo Hamisa Mobetto na Millard Ayo 

Mshindi wa   Milioni moja  mkazi Lucas Mtei wa Dar es Salaam amesema  fedha hizo zitamsaidia kuongeza mtaji wake wa biashara  kwani yeye ni mjasiriamali

Naye Angel Samwel mshindi wa milioni moja ameongezea kwa kusema  fedha hizo zitamsaidia kuongeza kwenye mtaji wa biashara yake 

Sanjari na hayo washindi wengine ambao ni Maua Ally, Raymond January, Milka Sanga,Mwajabu Mbwana wamesema fedha hizo zitawasaidi kwenye biashara zao na mambo binafsi

Promosheni hiyo ya chawote itadumu kwa siku tisini hii ikiwkuishaa  ni wiki ya tisa mshindi wa mwisho wa mwezi anashinda milioni tano mbali na zawadi za fedha taslim wanazotoa nyingine ni bonus,dakika na sms zikiwa zimesalia wiki nne promotioni hiyo kuweza .



Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



BBC NEWS