Na Matukio Daima App,Iringa
ASKOFU wa kanisa la kiinjili la kilutheri Tanzania (KKKT) dayosisi ya Iringa Dkt Blaston Gavile (pichani)amesema suala la ajira kwa sasa limekuwa ni changamoto kubwa serikalini hivyo njia pekee ya kupambana na tatizo la ajira ni vema kila moja kujiajili katika sekta binafsi .
Alisema kuwa badala ya kutegemea ajira kutoka serikali ni vema kila mmoja kufanya kazi kupitia sekta binafsi kama kilimo cha Parachichi , ufugaji na nyingine nyingi.
Alisema suala la ajira kwa sasa limekuwa ni gumu zaidi kutokana na uhitaji wa ajira kuwa mkubwa na serikali haiwezi kuajiri kila mmoja wetu .
Pamoja na kutoa wito wa kila mtanzania kuacha kutegemea ajira serikali askofu Dkt Gavile awataka waumini wa kanisa hilo na watanzania kwa ujumla kuendelea kuliombea Taifa na viongozi wote akiwemo Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ili kuliongoza Taifa katika misingi bora inayozingatia katiba na utawala bora .
Askofu Dkt Gavile alitoa wito huo Leo wakati akitoa salam za Pasaka kwa waumini wa Dayosisi ya Iringa katika ibada iliyofanyika usharika wa Kanisa kuu Iringa .
Kuhusu mmomonyoko wa maadili alisema kuwa hali halisi ya mmomonyoko wa maadili ndani ya mkoa wa Iringa na Taifa si njema kwani kila siku matukio ya ulawiti ,ushoga na usagaji yameendelea kuripotiwa jambo ambalo halikubaliki katika jamii .
“ Kazi yetu sisi wa Kristo ni kukemea vitendo hivyo visivyompendeza Mungu na kuomba toba ili aturehemu kuondokana na mambo hayo yasiyompendeza Mungu ukisoma Mwanzo sura ile ya 18 hadi 19 inaeleza jinsi ambavyo Ibrahimu alivyoomba toba kwa ajiri ya Sodoma na Gomola ambao waliadhibiwa kwa ajili ya Dhambi lakini nae Ibrahim alizidi kusimama katika Bwana “
Alisema pamoja na kumuomba Mungu bado wazazi na jamii inawajibu wa kuendelea kuongeza ulinzi kwa Watoto ili nao waweze kutimiza ndoto na malengo yao .
Mafundisho ya Uzushi kuwa siku hizo kumeendelea kuibuka mafundisho ya uzushi ambayo yanakaza zaidi mafanikio ya kiuchumi pasipo kufanya kazi na kuelekea watu kutangatanga kutafuta mahubiri hayo ambayo mwisho wa siku yanawapeleka kubaya zaidi .
Alisema hakuna mafaniko pasipo kufanya kazi hivyo ni vema kila mmoja kutambua mafaniko ya kweli ni kufanya kazi sio kutegemea wazushi na wapotoshaji wa maandiko ya Mungu .
Aidha Askofu Dkt Gavile aliwataka waumini wa kanisa hilo wanaposherekea sikukuu ya Pasak ana wakati wote kuendelea kuomba kwa ajili ya viongozi wa nchi akiwemo Rais , makamu wa Rais , waziri mkuu na spika wa Bunge ili waongozi nchi vema .
0 Comments