Header Ads Widget

WATUMISHI TRA WATAKIWA KUTANGULIZA UZALENDO KATIKA UKUSANYAJI KODI NJOMBE

 Na Gabriel Kilamlya Matukio DaimaAPP NJOMBE

Watumishi wa mamlaka ya mapato Tanzania TRA wametakiwa kuacha vitendo vya udanganyifu wakati wa ukadiliaji wa kodi kwa wafanyabiashara kwani vinasababisha serikali kukosa mapato mengi.


Katibu tawala Wilaya ya Njombe Emmanuel George  kwa niaba ya mkuu wa mkoa katika maadhimisho ya wiki ya shukrani kwa mlipa kodi amesema TRA wanapaswa kuonyesha uzalendo kwa kuacha vitendo vya kuingia makubaliano na wafanyabiashara kuiibia Serikali mapato.


Aidha  Bwana George amewataka TRA kuwaeleza wananchi kodi zao zinafanya nini na Kuna faida gani na hasara gani za kulipa  na kutolipa kodi.


Kamanda wa polisi mkoa wa Njombe Hamis Issa amesema kinachotakiwa katika ukusanyaji kodi ni uzalendo kwa watumishi wenyewe,Wananchi na hata wafanyabiashara hivyo kila mmoja anapaswa kuwajibika katika majukumu yake.











Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI