Header Ads Widget

RAIS SAMIA ASEMA UWEZEKANO NI KUPUNGUZA TOZO NA SIO KUONDOA DARAJA LA KIGAMBONI

 


Wakati Mbunge wa Kigamboni, Dk Faustine Ndugulile akiiomba Serikali kuangalia upya tozo katika Daraja la Kigamboni, Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuendelea kutozwa akiwataka wananchi wajenge mazoea hayo.


Katika msisitizo wake, Rais Samia amesema tozo hiyo inatokana na deni la gharama za ujenzi wa mradi huo hivyo hakuna mwingine wa kulipa isipokuwa wananchi wenyewe.


Awali, akitoa salamu katika hafla ya uzinduzi wa mradi wa maji Kigamboni, ugawaji vifaa vya uchimbaji visima na makabidhiano ya eneo la bwawa la Kidunda kwa mkandarasi Sino Hydro, Dk Ndugulile amemuomba Rais Samia kuangalia utaratibu wa kutoa tozo hiyo.

 

“Kigamboni unaingia kwa hela kila siku na lazima urudi kwa hela, kwa hiyo hili nalo Mheshimiwa Rais kama nalo unaweza kwenda kuliangalia nitashukuru sana,” amesema.


Akijibu hilo katika hotuba yake, Rais Samia amesema uwezekano uliopo ni kupunguza tozo hiyo, lakini si kuiondoa kabisa.


“Ni kweli Daraja la Kigamboni tunatoa tozo lakini hii imetokana na mradi wenyewe ulivyojengwa. Daraja la Kigamboni ni mkopo na kama ni mkopo lazima tuurudishe na hakuna wa kurudisha zaidi ya sisi wenyewe wananchi ni uzoefu wa kwanza kuona wananchi wanalipa kupita pale,” amesema.


Ameeleza baadhi wanafananisha mradi huo na Daraja la Tanzanite, akifafanua kinachotozwa kwenye mradi wa Julius Nyerere kinatokana na deni lililopo, wakati daraja la Tanzanite limejengwa kwa fedha ya Serikali.


“Wengine walisema mbona daraja la Tanzanite watu hawalipishwi, Tanzanite ni fedha ya Serikali asilimia 100, daraja la Kigamboni ni mkopo lazima urudishwe, lakini nataka niseme wananchi sasa mzoee huduma za namna hii na barabara za namna hii zitakuja nyingi.


“Ile kila kitu bure kidogo kidogo itakuwa inaondoka, ili tuiendelee lazima tuwe na barabra, madaraja na vivuko vizuri na hayo yataletwa na sekta binafsi ili iendelee lazima tulipie hiyo huduma, kwa hiyo tozo tunaweza kuangalia kuipunguza lakini sio kwa kuiondosha,” Rais Samia.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI