Header Ads Widget

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII APONGEZA CHUO CHA CDTI IRINGA ATOA AGIZO KWA VYUO VINGINE


Naibu Waziri  Maendeleo ya Jamii, Jinsia,wanawake na makundi maalumu Mhe. Mwanaidi Ali Khamis amepongeza chuo Cha maendeleo ya Jamii Ruaha mkoani Iringa Kwa mapambano dhidi ya udumavu na utapiamlo .

Akitoa pongezi hizo Leo wakati wa Mahafali ya 14 ya chuo hicho Naibu Waziri huo amesema jitihada kubwa zimefanywa na chuo hicho Katika utoaji elimu ya lishe Kwa jamii inayozunguka .


Hata hivyo amepongeza menejimenti ya chuo Kwa kuendelea kuimalisha Mapato ya ndani Kwa kubuni vyanzo vya Mapato kama ugugaji samaji ,uchakataji ngozi na shughuli nyingine za Kiuchumi .

Alisema alipofika chuoni hapo alitembelea mabwawa ya samaki na kuona jitihada hizo kubwa ambapo kupitia ugugaji huo wananchi watapata Afya Bora .


Aidha alipongeza chuo Kwa kupata kibali Cha utafiti wa lishe Iringa na kuagiza vyuo vingine kuandika maandiko ya kazi mbali mbali za chuo Kwa lengo la Kutangaza chuo .


Akielezea changamoto za chuo hicho kama Nyumba za walimu na Mabweni alisema changamoto hizo amezichukua na atakwenda kuzifanyia kazi .

Pia alisema suala la miundo mbinu ya barabara atauagiza uongozi wa mkoa ili kuboresha mazingira ya chuo hicho .


Huku akiwataka wahitimu wa chuo hicho kutumia vema mafunzo ambayo wamepata Kwa kwenda Vijijini kuwatumikia wananchi.

Alisema Rais  Samia Suluhu Hassan ameunda wizara ya maendeleo ya Jamii ili kusaidia jamii kupata elimu Bora .

"Ndugu wahitimu mtakapopata fursa ya kupata kazi jiepusheni na vitendo vya Rushwa na miawe mabalozi mazuri wa kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia"


"Tumekuwa tukifanya kazi kwa ushirikiano wa karibu na nimekuwa mstari wa mbele katika kuunga mkono juhudi za Chuo katika utekelezaji wa majukumu yake, ninaahidi kutimiza wajibu wangu nikiwa kama Naibu Waziri, kwa kutoa msaada pale itakapohitajika na nitakapoona inafaa".

Alisema anatambua kuwa  ili kuweze kufikia malengo waliyojiwekea katika kutekeleza mpango mkakati wa Chuo, ni lazima kuwe na juhudi za makusudi za kuhakikisha upatikanaji wa fedha za maendeleo.

" Nitajitahidi kwa kadri ya uwezo wangu kwa kushirikiana na Wizara yetu pamoja na Wizara ya Fedha kuhakikisha suala la upatikanaji wa fedha za kutosha za ruzuku na miradi ya maendeleo kwa ajili ya uendeshaji wa Chuo hiki linapewa kipaumbele Ndugu Wahitimu, Napenda nitumie fursa hii kuwapongeza sana wote ambao mtatunukiwa hivi punde Stashahada na Astashahada za Maendeleo ya Jamii. Niwapongezeni sana kwa juhudi kubwa mliyoonyesha katika kipindi chote mlichokuwa hapa Chuoni,  kilichowapelekea kufikia mahafali ya siku ya leo"

Aidha alisema anatambua umuhimu wa elimu ya Maendeleo ya Jamii katika maendeleo ya ulimwengu wa sasa; napenda niwasisitize umuhimu wa kujiendeleza katika fani hii ili muweze kuwa chachu ya mabadiliko chanya ya kimtazamo wa jamii.


Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan anachukizwa Sana na vitendo vya ukatili vinavyojitokeza Katika jamii yetu hivyo ni jukumu lenu kwenda kulifanyia kazi janga la ukatili Kwa kutoa elimu Bora na wale wanaopata msongo wa mawazo Kwa kufanyiwa vitendo vya ukatili mkawasaidie kuwapa elimu.

Awali mkuu wa chuo hicho Godfrey Mafungu alipongeza Serikali Kwa kuendelea kutoa fefha za maboresho Katika chuo hicho na kuwa pamoja na jitihada hizo kuwa zipo changamoto za Nyumb a za walimu na ma b mabweni. 





























































Chuo cha Maendeleo ya Jamii Ruaha kilianzishwa mnamo miaka ya 1960 kwa kutoa mafunzo ya kilimo kikiwa chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu. Mwaka 2002 Chuo kilibadilishwa kutoka Chuo cha Kilimo na kuwa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi (Folk Development College- FDC) na kuanza kutoa mafunzo ya ufundi katika fani mbalimbali zikiwemo za Useremala, Uashi, Ushonaji, Ufundi Magari, Upishi, Ufundi Umeme wa Majumbani na Mbinu bora za Kilimo. Mabadiliko hayo yalibadilisha muundo wa kimamlaka ambapo Chuo kilihama kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu na kuwa chini ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto.  Mwaka 2008 Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto iliamua kukibadilisha chuo hiki na kuwa Chuo cha Maendeleo ya Jamii na kuanza kutoa mafunzo ya Maendeleo ya Jamii katika ngazi za Astashahada na Stashahada. 
1.2 USAJILI NA ITHIBATI
Mheshimiwa Mgeni Rasmi, Chuo kilisajiliwa mwaka 2012 kwa namba ya usajili PWF/028 na lililokuwa Baraza la Taifa la Elimuya Ufundi (NACTE) kwa sasa linajulikana kama Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTEVET). Tarehe 25 Oktoba, 2019 Chuo kilipata ithibati kamili (Full Accreditation) ambapo Baraza liridhia kuanza kutolewa kwa mafunzo ngazi ya stashahada ya maendeleo ya jamii.  
1.3 ENEO  NA MAHALI CHUO KILIPO 
Mheshimiwa Mgeni Rasmi, Chuo cha Maendeleo ya Jamii Ruaha kipo Mtaa wa Chuo, Kata ya Ruaha, Tarafa ya Iringa Mjini, Halmashauri ya Manispaa ya Iringa, Mkoa wa Iringa, ikiwa ni takribani kilomita tano (5) kutoka makao makuu ya Manispaa ya Iringa. Chuo kina eneo lenye ukubwa wa hekta 37.42 ambalo limepimwa na kupatiwa hati miliki.

Chuo kimeweza kupata mafaniko yafuatayo

Ujenzi wa ukumbi wa mihadhara wenye uwezo wa kuchukua wanachuo 260, Mabweni mawili yenye uwezo wa kuchukua wanachuo 128 na maktaba yenye uwezo wa kuchukua wanachuo 144 kwa awamu moja;
Uanzishwaji wa Dawati la Jinsia kwa ajili ya kukabiliana na ukatili wa kijinsia.
Utekelezaji wa programu ya Ushirikishwaji jamii, Uanagenzi na kituo cha ubunifu na maarifa ikiwa ni utekelezaji wa ilani ya chama cha mapinduzi ibara 229
Uwepo wa miradi ya uzalishaji mali kwa lengo la kutoa mafunzo na kuongeza mapato ya ndani ya Chuo
Kutekeleza taratibu za awali za kufanya utafiti wa hali ya Lishe na Udumavu katika Manispaa ya Iringa

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI