Header Ads Widget

WALIMU MAKADA WA CCM WACHANGIA DAMU KITUO CHA AFYA BUZURUGA.


Shirikisho la Walimu Makada wa Chama cha Mapinduzi mkoani Mwanza, wamechangia Damu katika Kituo cha Afya Buzuruga pamoja na kutoa misaada mbalimbali kwa Mama wajawazito na wagonjwa katika kituo hicho


Mwenyekiti wa Shirikisho la Walimu Makada wa CCM Jackson Kadutu amesema, wameamua kufanya zoezi la uchangiaji wa damu ikiwa ni kumuunga mkono Mheshimiwa  Rais Samia Suluhu Hassan ili kusaidia Mama Wajawazito na Watoto  katika changamoto ya uhaba wa damu kituoni hapo.


Naye Katibu wa Shirikisho la Walimu Makada wa CCM Devid Sulube amesema, kwa pamoja katika Shirikisho hilo wameweza kuchanga kiasi cha shilingi milioni mbili na kununua mahitaji mbalimbali kwa ajili ya kutoa msaada katika Kituo cha Afya Buzuruga kwa ajili ya Mama na Mtoto


 Afisa Tarafa ya Ilemela Suzana Tulimanywa amewapongeza walimu Makada wa CCM kwa kufanya zoezi  la kizalendo la uchangiaji damu pamoja na kutoa msaada wa vifaa mbalimbali kwa mama wajawazito na watoto huku akitoa rai kwa vyama vingine kuiga mfano huo.











Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI