Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe Prof. Adolf Mkenda amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe Simai Mohamed Said Ofisini kwake Jijini Dar es salaam.
Pamoja na mambo mengine katika mazungumzo hayo mawaziri hao wamekubaliana kufanya kazi kwa karibu zaidi katika kupitia Sera Elimu za Tanzania Bara na Zanzibar na mitaala ya Elimu Msingi.
Baada ya kikao hicho Mawaziri hao wamekubalina kuwa na kikao cha pamoja na wataalam na watendaji kutoka Wizara hizo mbili kitakachofanyika Zanzibar hivi karibuni ili kujadili utekekezaji.
0 Comments