Header Ads Widget

VIJANA MRADI WA YAM WAPEWA SOMO LA UTAJIRI WA ZAO LA PARACHICHI

 

Sadick Ngwiso Mkazi wa Kijiji Cha Luhunga Kitongoji Cha Igoda wilaya ya Mufindi mkoani Iringa akigema Ulanzi

Mkulima Mjasiriamali wa Kilimo cha Parachichi Katika Kijiji Cha Igoda wilaya ya Mufindi mkoani Iringa Aidan Kiwale amewataka vijana toka mazingira magumu ambao wapo kwenye mradi wa Youth Agency Mufindi (YAM) kuchangamkia fursa ya Kilimo cha Parachichi Kwa kuwa kinalipa .

Kiwale ametoa Rai hiyo jana  wakati wa mwendelezo wa Mafunzo ya Siku 10 ya Ujasiriamali yanayoendeshwa na Halmashauri ya Mufindi Kwa kushirikiana na mradi wa YAM pamoja na taasisi ya Foex Community and wildlife conservation (FCWC).

Amewataka vijana waache kukaa Vijiweni na badala yake kutumia vizuri muda Kwa kufanya kazi za Kilimo na nyingine za ujasiriamali ambazo wakizingatia zitawatoa Katika dimbwi la umasikini wa kipato 

Mkulima wa Parachichi Kijiji Cha Luhunga Aidan Kiwale akitoa elimu ya Kilimo hicho Kwa vijana mradi wa Youth Agency Mufindi

Awali akitoa ushuhuda wa jinsi alivyoanza Kiwale ambae ni mwenyekiti wa Serikali ya Kitongoji kwenye Kijiji Cha Igoda amesema mwanzo wananchi hawakumuelewa na walikuwa wakimuona kama amepitwa na wakati ila Sasa Kila mmoja anamuonea wivu Kwa pesa nzuri anayopata kwenye Kilimo cha Parachichi 

Alisema kupitia zao hilo la Parachini hivi Sasa anakipato Cha uhakika kutoka na mti mmoja wa Parachichi unamwezesha kupata fedha zaidi ya shilingi 400,000 Kwa mchumo mmoja na yeye ana zaidi ya miti 2000 ya Parachichi  hivyo Kwa mwaka anamiliki kipato Cha uhakika .

Alisema Kuhusu Soko la Parachichi ni zuri kwani Soko dogo la  Parachichi Kwa ajili ya Kusafirisha kwenda nje ya Nchi lipo mkoani Njombe na kuwa Kwa mkulima Mwenye uwezo anaweza Kusafirisha mwenyewe kwenda kuuza nje .

 

Hata hivyo akishukuru Kwa elimu hiyo mshiriki Fex  Kitinusa amesema elimu hiyo ni mtaji kwao na watakwenda kuitumia 

Halmashauri ya Mufindi chini ya taasisi ya FCWC ndio watekelezaji wa mradi huo Youth Agency Mufindi kupitia ufadhili wa Finland  ni mradi wa miaka minne utakaowafikia vijana 770 pamoja na watoto kwenye vijiji 16 vya kata za Luhunga , Mdabulo na Ihanu .

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI