Rais wa Africa Cotton Association amnaye pia ni mkurugenzi mkuu wa TCB
Marco Mtunga akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza amesema,
Jumuhiya ya pamba africa itafanya mkutano wa 18 jiji Mwanza katika ukumbi wa Malaika resort kuanzia machi 17 hadi 18 ambapo kila mwaka jumuhiya hiyo ukutana kufanya mkutano wa mwaka uku ikiundwa na makampuni ya nchi zote zinazolima pamba barani Africa
Aidha mkutano huo unatarajiwa kuhudhuliwa na wageni zaidi ya mia moja na ishilini kutoka nchi za Africa pia utahudhuliwa na makampuni ya kununua pamba duniani kote
Katika mkutano huo pamoja na kuzungumzia maendeleo ya kilimo cha pamba barani Africa pia umekuwa ukiwakutanisha wanunuzi wa pamba na wauzaji wa pamba
Mkutano huo ambao unatarajiwa kuwa wa siku mbili uku siku ya kwanza ikitumika kutoa taarifa za maendeleo ya kilimo hicho kwa bara la Africa hivyo Tanzania ikiwa mwenyeji wa mkutano itatoa taarifa yake jinsi kilimo cha pamba kinavyolimwa na inavyonufaisha uchumi wa nchi ya Tanzania .
0 Comments