WAZIRI wa Elimu Sayansi na Teknolojia Profesa Adolf Mkenda amegawa jumla ya Kompyuta 300 kwa vyuo vya ualimu huku akisema mgao huo umezingatia uwiano kati ya wanachua na vifaa vilivyopo katika vyuo kwa sasa.Mwandishi Hamida Ramadhan Dodoma
Ameyasema hayo leo jijini hapa wakati akikabidhi Kompyuta kwa vyuo vya ualimu Kompyuta za Mezani na Kompyuta Mpakato ambapo Amesema Jumla ya Kompyuta 300 zitakazogaiwa kwa vyuo 13. Vyuo 4 vitapata Kompyuta 30 na Vyuo 09 Kompyuta 20.
Aidha, vyuo vyote 35 vitapatiwa Kompyuta Mpakato 1 kwa ajili ya kusaidia idara
zenu vyuoni.
" Kompyuta hizi zimenunuliwa kwa gharama kubwa hivyo naagiza kila Mkuu
wa Chuo kuhakikisha kuwa zinatumika kwa malengo ya kuimarisha
ufundishaji na ujifunzaji Chuoni," amesema Waziri Mkenda
Hata hivyo amewataka Kila Mkuu wa Chuo kuhakikishe mali zote
za Serikali zinatunzwa ipasavyo ili kuleta tija ya fedha zilizotumika vyuo
vyote vya Ualimu vizingatie matumizi sahihi ya kompyuta hizi ikiwemo kuhaikikisha ziko katika mazingira yaliyo safi na salama kama ilivyo kanuni
na taratibu za kutunza na kuhifadhi vitu vyaTEHAMA.
"Mtakumbuka kuwa, Wizara imekwisha gawa vifaa vya TEHAMA ikiwa ni
Kompyuta za Mezani (Desktop) 1,120, Kompyuta za mkononi au
Kompyuta Mpakato (laptop) 113, na Projekta 186," amesema Waziri Mkenda
Ameeleza kuwa Vifaa hivi viligawiwa kwa Vyuo vyote 35 vya Ualimu, hivyo vifaa vya leo ni nyongeza ili kukidhi
mahitaji. Hii itasaidia kupunguza uwiano wa matumizi ya kompyuta kwa
Wanachuo kutoka Wanachuo 28 kwa Kompyuta 1 (28 :1) hadi kufikia
Wanachuo 2 kwa Kompyuta 1 (2 :1) vyuoni.
Amesema wa matumizi ya vifaa na mifumo hiyo ya TEHAMA iliyoboreshwa inahitaji pia kuwepo kwa Mtandao imara, hivyo, Wizara itaviunganisha Vyuo vyote
vya ualimu katika Mkongo wa Taifa ili kuhakikisha kuwa Vyuo vinaweza
kupata mtandao imara utakaowawezesha Wakufunzi na wanachuo kutumia ufundishaji na ujifunzaji kwa ufanisi.
" Kwa mwaka huu tunatarajia
kuunganisha Vyuo 15 vya Ualimu katika Mkongo wa Taifa Kazi ya
Kuunganisha Vyuo hivyo inaanza leo tarehe 21/02/2022 baada ya Wizara
kuwakabidhi wakandarasi wawili (BM Telecommunication na SoftNET
Solution)," amesema
Awali akisoma taarifa ya Mradi wa kuendeleza elimu ya ualimu (TESP) Kaimu Katibu Mkuu wizara ya Elimu Caroline Nombo amesema mradi namba 4323 katika horodha ya mradi inayotekelezwa na serikali mradi unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya serikali ya jamhuri ya ya Tanzania kupitia wizara ya Elimu na serikali ya Canada kupitia ubalozi wake hapa nchini.
Amesema Mchango wa serikali ya Canada katika mradi huo ni jumla ya Dola za KiCanada shilingi milioni 53 mchango wa serikali ya Tanzania ni kugharamia shughuli mbalimbali za uendeshaji wa vyuo zikiwemo gharama za malipo ya chakula kwanavyuo na gharama zamafuzo ya vitendo kwa walimu .
"Dhumuni kuu la mradi huu ni kuendekeza elimu ya ualimu hapa nchini kwa kuboresha mazingira ya ujifunzaji na ufundishaji wanufaika wa mradi huo ni vyuo vyote vya serikali 35 ofisi ya tamisemi taasisi ya elimu tanzania baraza la mitihani tanzania wakala wa maendeleo ya uongozi wa elimu," amesema Kaimu katibu mkuu huyo
Malengo kuimalisha miundombinu na mifumo ya tehama katika vyuo vyote vya ualimu 35.
Mwisho
0 Comments