Header Ads Widget

WANANCHI WATAKIWA KUEPUKANA UTUMIAJI WA DAWA KIHOLELA

 



WANANCHI  wametakiwa kuepukana na utumiaji wa dawa kiholela kwani utumiaji madawa holela usababisha madhara makubwa kwa afya ya binadamu.....Na Hamida Ramadhan Dodoma 


Mbali na kuwataka wanachi kutokutumia dawa kiholela wametakiwa kutonunua madawa katika maduka ya madawa muhimu ya binadamu ambayo hayajasajiliwa na baraza la Famasi .


Hayo yameelezwa na Msajli wa Baraza la Famasi Elizabeth Shekhalaghe alipokuwa akizoa taarifa ya kwa Umma kuhusu matumizi holele ya dawa.


Sambamba na hayo wamiliki wote wenye wenye maduka ya dawa wanatakiwa kuhusha leseni zao ambapo mwisho wa kuhuisha ni Desemba 31 mwaka huu vinginevyo wasiofanya hivyo watafutiwa leseni.


Amesema kuwa pia ni marufuku mmiliki wa duka la dawa kuweka matangazo ya kujitangaza na kwa kuweka mabango ya matangazo matangazo ni kosa kisheria.


Ameeleza kuwa kutokana na majukumu ya Baraza la Famasi wananchi wanapaswa kuelewa kuwa dawa ni nini na matumizi sahihi ya dawa ni nini  ili kila anayetumia basi aweze kuelewa umuhimu huo na athari zake.


"Kwa kifupi, dawa ni kemikali au kitu chochote kinachotumika kutibu, kuzuia au kutambua magonjwa ya binadamu au wanyama. 




Amesema  matumizi  sahihi  ya  dawa  yanajumuisha mgonjwa  kufanyiwa  uchunguzi  wa  kina, kuandikiwa na kupewa dawa inayostahili kulingana  na  hali  ya  ugonjwa  alionao kwa kutumia  kiasi  sahihi,  kwa  njia  sahihi  na kwa muda muafaka kama alivyoelekezwa na mtaalam wa afya.



"Nitoe wito kwa wananchi kutambua kwamba Dawa ni sumu  na huleta madhara iwapo hazitatumika ipasavyo hivyo ni muhimu kuzingatia matumizi sahihi ya dawa na ushauri wa wataalamu kwa matokeo mazuri ya tiba za magonjwa yanayowakabili," amesema 



Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI