Header Ads Widget

BEI YA MAEGESHO YA MAGARI, KUPITIA TeRMIS YASHUSHWA



Na Fatma Ally MDTV Dar es Salaam


Serikali Kupitia Wizara Ofisi Ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa (TAMISEMI) imeshusha bei za maegesho ya magari ambapo kwa saa mtu atatakiwa kulipa tozo ya kiasi cha Tsh  500 na Tsh  2500 kwa siku kutoka Tsh  4000.


Aidha, imeridhia kurudisha mfumo wa ukusanyaji Ushuru wa Maegesho kwa njia ya kielektroniki (TeRMIS) uanze kutumika tena kuanzia tarehe 1 Desemba, 2021 katika maeneo yote ambapo mfumo huo umefika.


Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Ummy Mwalimu mtumiaji wa maegesho sasa atatakiwa kulipa ushuru ndani ya siku 14 badala ya siku 7 tangu alipotumia maegesho na endapo atashindwa kulipa ndani ya muda huo atatakiwa kulipa Ushuru wa Maegesho pamoja na faini ya shilingi 10,000 badala ya shilingi 30,000 zilizokuwa zikitozwa awali, ambapo adhabu wa shill 30,000 ameifuta.


Amesema kuwa, hadi sasa TARURA kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais TAMISEMI tayari wamezifanyia kazi changamoto zilizojitokeza katika matumizi ya mfumo wa kielektroniki wa ukusanyaji ushuru wa maegesho ambapo ilikuwa changamoto kwa watumiaji.


“Ukusanyaji wa Ushuru wa Maegesho ya magari kwa kutumia mfumo wa TerMIS utapunguza mianya ya upotevu wa mapato ya Serikali na kuwezesha fedha hizo kuingia moja kwa moja Serikalini. Kutokana na umuhimu wake ninarejesja matumizi ya Mfumo huu kuanzia tarehe 1 Desemba 2021”. Amesema Waziri Ummy.


Aidha, amesema miongoni mwa changamoto ambazo wamezifanyia kazi ni pamoja na Wateja kutopatiwa taarifa za kudaiwa ushuru wa maegesho kwa wakati, Kiwango kikubwa cha gharama za maegesho, Muda wa kulipa ambapo hapo awali mtumiaji wa maegesho alitakiwa kulipa ushuru ndani ya siku 7 tangu alipotumia maegesho na endapo atashindwa kulipa ndani ya muda huo alipaswa kulipa mara mbili ya ushuru aliokuwa anadaiwa. Na endapo atazidisha siku 14 pia alitakiwa Ushuru wa Maegesho pamoja na faini ya shilingi 30,000.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI