Header Ads Widget

KAFULILA AWATAKA WAKANDARASI WA BARABARA KUTEKELEZA MIRADI KWA KIWANGO KIZURI.



Na Costantine Mathias, Maswa.


MKUU wa Mkoa wa Simiyu David Kafulila amewataka wakandarasi wanaotekeleza miradi ya barabara mkoani humo kujenga kwa kiwango kizuri pia kuonesha thamani ya fedha vinginevyo watakosa sifa ya kutekeleza miradi hiyo.


Aidha Kafulila amesema suala la usimamizi wa miradi ya maendeleo ikiwemo barabara ni kwa viongozi wote wakiwemo viongozi wa CCM ambapo pia amezitaka taasisi za serikali kutoa taarifa utekelezaji wa miradi yao kwa viongozi wote pamoja na vyombo vya Habari.



Kafulila ameyasema hayo leo mara baada ya kukagua ujenzi wa wa kipande cha lami ya Maswa-Mwigumbi chenye urefu wa kilometa 15 ambacho kilejengwa chini ya kiwango.


Amesema barabara ikijengaa chini ya kiwango itatumia fedha nyingi za ukarabati, na kwamba mkandarasi akifanya vibaya atakosa sifa na nafasi ya kuendelea kufanya kazi itapungua.



"Barabara ya lami ya kilometa 1 inatumia zaidi ya bilioni 1, lazima tusimamie kaa ukaribu ili thamani ya fedha iweze kuonekana...suala la usimamizi wa miradi ni la wote, CCM wakitaka taarifa wapeni" amesema Kafulila.


Awali Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS) Mkoa wa Simiyu Mhandisi John Mkumbo amesema Barabara ya Maswa-Mwigumbi yenye urefu wa Kilometa 50.3 ilikuwa inatekelezwa na mkandarasi CHICO GROUP Co. Ltd kwa gharama ya bilioni 61.4.


Amesema baada ya mradi kukamilika haukupokelewa kutokana na baadhi maeneo kutokamilika vizuri, na kwamba walibaini kilometa 3.6 upande wa Simiyu na kilometa 5 upande wa Shinyanga hazikujengwa kwa kiwango kizuri.


"Zimeongezeka na kufikia kilometa 15 baada ya uchunguzi zinazohitajika kurudiwa, mkandarasi yuko eneo la mradi na mwezi Disemba atakabidhi mradi" amesema Mhandisi Mkumbo.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI