Header Ads Widget

MWENYEKITI WA SERIKALI AMBE NI MC MAARUFU AJIUA KWA KUJINYONGA BAADA YA KUUA MKE KWA WIVU WA MAPENZI

Picha   hii  ni  mfano  tu haina  uhalisia na tukio husika

Mwenyekiti  wa serikali  ya  kitongoji cha  Urua kijiji  cha Mfuruashe  wilaya  ya  Rombo mkoani  Kilimanjaro  ambae ni mshereheshaji  (MC)  maarufu Augustine Moshi (35) atuhumiwa kumuua  mkewe  Anastasia Augustine (31) kwa  kumkatakata na  kitu chenye ncha kali   kabla ya  yeye  mwenyewe  kuchukua uamuzi wa  kujinyonga kutokana na  kile kinachodaiwa ni  wivu  wa  mapenzi.

Imeelezwa  kuwa  mwenyekiti  huyo  ambae  pia ni MC maarufu katika wilayani  Rombo anadaiwa  kutenda unyama huo  usiku  wa kuamkia Novemba 8 mwaka huu 2021.

Akithibitisha kutokea kwa  tukio hil,o  mkuu  wa  wilaya ya Rombo  ambae ni  mwenyekiti wa  kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya  Kanali Hamis Maiga alisema  kuwa  wanandoa hao  walikuwa  na mgogoro  wa  kimapenzi  ambapo  wiki   moja iliyopita  mke  alipeleka malalamiko yake dawati la  jinsia wilaya ya  Rombo .

Baadhi ya  wananchi  wa  kitongoji   hiyo akiwemo Amina Ally  walieleza  kusikitishwa na tukio  hilo na  kuwa hata kama  mmoja  wapo  alikuwa na tatizo katika  ndoa dawa  haikuwa ni  kuchukua uamuzi kama  huo bali  walipaswa  kumaliza  tofauti  zao nje ya maamuzi hayo .


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI