Header Ads Widget

MKURUGENZI KAMPUNI YA RICK BRIAN KIKOTI ATANGAZA NEEMA WANAFUNZI UPETA SEKONDARI KUULA


Mkurugenzi wa kampuni ya Rick na mzaliwa wa kata ya Bomalang'ombe kijiji cha Ng'ingula wilaya ya Kilolo mkoani Iringa Brian Kikoti ameahidi kutatua changamoto ya maji katika shule ya sekondari Ipeta .

Kikoti akiwa mgeni rasmi kwenye mahafali ya kidato cha nne shule ya Sekondari Ipeta iliyoko kata ya Bomalang'ombe alitoa ahadi hiyo baada ya wahitimu wa kidato cha nne shuleni hapo kwenye risala yao kueleza changamoto hiyo ya maji 

"Kama gharama za kuchimba kisima ni hizi basi mimi Nasema kuanzia kesho mafundi wafike hapa na kisima kianze kuchimbwa" 

Kuhusu taaluma shuleni hapo  kikoti aliwataka  walimu, wazazi na wanafunzi kushirikiana na kila mmoja kutimiza wajibu wake ili kuimarisha ufauru wa wanafunzi shuleni hapo.

Akielezwa kuhusu  suala la motisha kwa wahitimu wa kidato cha nne, Kikoti ameahidi kutoa kiasi cha shilingi laki tatu kwa kila mwanafunzi atakayepata Daraja la kwanza katika matokeo  ya mtihani wa kuhitimu kidato cha nne mwaka huu na kwamba hata kama watakuwa zaidi ya arobaini atawapa wote.

Kwa upande wake mkuu wa shule hiyo pamoja na  Diwani  viti maalum, wazazi pamoja na wanafunzi wamempongeza  Kikoti kwa kwa moyo wake wa kujitolea na kukumbuka kuchangia maendeleo ya nyumbani aliko zaliwa.


Kikoti ametoa ahadi hiyo huku   zikiwa zimepita siku chache tu baada ya  kuchangia ujenzi wa jengo la ofisi ya kata ya Lugalo wilayani Kilolo, ambapo aliahidi kuendelea kuchangia maendeleo maeneo mengi katika wilaya ya  Kilolo na mkoa wa Iringa kwa ujumla.

 Kwa upande wao wageni walioambatana na  Kikoti ,Baraka Kimata diwani mstaafu kata ya Kitwiru na Bw Osca Ndale wamemuunga mkono kwa kuchangia mifuko 10  ya saruji ambapo waliahidi kumkabidhi mkuu wa shule wakati  wowote atakapo kuwa tayari kuichukua.








Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI