![]() |
Tarehe 17 Februari 2022, Rais Samia Suluhu Hassan alipokuwa katika ziara barani Ulaya kwa mkutano uliowakutanisha viongozi wa Umoja wa Ulaya (EU) na Umoja wa Afrika (AU), nilipokea ujumbe kupitia watu wangu kwamba alikuwa anataka kuonana nami.
Wakati huo, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, alikuwa gerezani kwa takribani miezi sita au saba akikabiliwa na kesi ya ugaidi.
Nilipopata ujumbe huo, nilishauriana na viongozi wenzangu. Tuliona ilikuwa ni hatua nzuri, hivyo nikaenda kukutana naye. Aliniambia alikuwa na nia ya kuyamaliza matatizo yaliyokuwa yamejitokeza wakati wa utawala uliopita.
Nikamwambia aanze kwa kumwachilia Mwenyekiti wetu, Freeman Mbowe, ndipo mazungumzo mengine yaweze kuendelea. Pia nikasema tunahitaji kuzungumzia Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi. Alijibu kuwa alikuwa tayari kufanya mazungumzo hayo.
Aidha, nilimweleza kuwa mimi, Godbless Lema na wengine tulikuwa tumekimbia nchi kutokana na hofu ya usalama wetu, hivyo tulihitaji uhakikisho kwamba ilikuwa salama kurejea nyumbani. Baadaye, alitangaza bungeni kuwa Watanzania waliokuwa uhamishoni warejee nchini. Mbowe naye aliachiwa huru, jambo lililotupa faraja ya kurudi nyumbani.
Tuliporejea, tulipendekeza kuwa watu wote waliokuwa wamefunguliwa kesi ambazo tuliamini zilikuwa na misingi ya kisiasa wafutiwe mashtaka, na baadhi ya kesi hizo zilifutwa.
Baadaye yakaanza mazungumzo kati ya CHADEMA na CCM. Tulipeleka mapendekezo mbalimbali kuhusu Katiba Mpya, muundo wa Tume Huru ya Uchaguzi na ratiba ya utekelezaji wa mageuzi hayo.
Kwa upande wetu, tulitaka mchakato wa Katiba Mpya ukamilike kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2025. Hata hivyo, tulianza kuona hakuna hatua za kutosha zilizokuwa zinachukuliwa. Mara nyingi tuliwasilisha mapendekezo kwa maandishi lakini majibu yalitolewa kwa njia ya mazungumzo badala ya maandishi rasmi.
Takribani mwaka mmoja ulipita bila majibu rasmi ya maandishi kuhusu mapendekezo yetu.
Mwaka 2025, tuliendelea kusisitiza kuwa majibu yatolewe kwa maandishi ili kuwe na uwazi kuhusu mambo yaliyokubaliwa na yaliyokataliwa.
Tarehe 21 Mei 2025, tulipokea majibu ya maandishi yaliyokataa mapendekezo yetu yote.
Baada ya hapo, tulikaa na kujiuliza maana ya maridhiano ikiwa hakuna makubaliano yanayotekelezwa zaidi ya vikao vya mazungumzo. Tukafikia hitimisho kwamba ni lazima kurejea kwa wananchi.
Tarehe 31 Mei 2025, tuliamua kama chama kuanzisha kampeni ya kuhamasisha madai ya Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi. Tulizunguka nchi nzima kuzungumza na wananchi kuhusu masuala hayo.
Kadiri joto la kisiasa lilivyoongezeka, ndivyo madai ya kukamatwa kwa wanachama na viongozi wa upinzani pamoja na kesi mbalimbali yalivyoendelea kujitokeza.
Hali hiyo iliendelea hadi uchaguzi wa serikali za mitaa na vijiji wa Novemba 2024.
Ndani ya chama kulikuwa na mjadala mkubwa kuhusu kushiriki au kutoshiriki uchaguzi huo kutokana na kutokuwepo kwa mageuzi yaliyokuwa yanadaiwa. Hatimaye, CHADEMA iliamua kushiriki.
Lissu alidai kuwa uchaguzi huo ulisimamiwa na mfumo wa utawala wa serikali kupitia TAMISEMI, huku watendaji mbalimbali wa uchaguzi wakiwa ni wateule wa mamlaka ya serikali.
Pia alidai kuwa wagombea wengi wa upinzani walienguliwa katika maeneo mbalimbali ya nchi, hali ambayo, kwa mujibu wake, iliathiri ushindani wa kisiasa katika uchaguzi huo.
Lissu alidai kuwa wagombea wengi wa upinzani walienguliwa katika maeneo mbalimbali ya nchi, hali ambayo, kwa mujibu wake, iliathiri ushindani wa kisiasa katika uchaguzi huo.
Alisema waliopinga matokeo hayo walikumbana na nguvu za dola katika maeneo mbalimbali, akidai kuwa watu kadhaa waliuawa Tarime.
Baada ya uchaguzi huo wa Novemba 28, wiki iliyofuata, tarehe 3 Desemba, Kamati Kuu ya CHADEMA ilikutana kujadili hatua za kuchukua kufuatia yaliyotokea katika uchaguzi na mazingira ya kisiasa yaliyokuwepo nchini.






0 Comments