Israel inasema haikuhusika na mashambulizi yaliyosababisha vifo vya walinda amani wawili wa Umoja wa Mataifa kusini mwa Lebanon siku ya Jumatatu.
Matokeo ya awali ya uchunguzi wa Kikosi cha Muda cha Umoja wa Mataifa nchini Lebanon (Unifil) yanaonyesha kuwa "mlipuko wa barabarani" ulipiga msafara karibu na Bani Haiyyan, na kuwaua walinda amani wawili wa Indonesia na kujeruhi wengine wawili.
Jeshi la Ulinzi la Israel (IDF) linasema tukio hili "halikusababishwa na shughuli za IDF".
"Uchunguzi wa kina unaonyesha kwamba hakuna kifaa cha kulipuka kilichowekwa katika eneo hilo na wanajeshi wa IDF, na kwamba hakuna askari wa IDF waliokuwepo katika eneo hilo hata kidogo," inasema katika taarifa.
Inaongeza kuwa inalenga maeneo ya Hezbollah katika eneo hilo, sio Unifil, na iliitaka Unifil "kuepuka kuwepo katika maeneo ya mapigano" ambayo IDF imetoa maagizo kwa watu kuhama.
MWISHO





0 Comments